Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi (Head of Consumer Banking), Stephen Adili (wa pili kushoto) akimkabidhi Mshindi wa BSS 2021 (Bongo Star Search), Yohana Braison Mwayinga, kitita cha shilingi milioni kumi (10,000,000/-) ikiwa ni zawadi ya mshindi wa kwanza, katika hafla fupi ya makabidhiano hayo iliyofanyika leo kwenye tawi la Benki ya CRDB la Azikiwe, jijini Dar es salaam. Wapili kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya BenchMark ambao ndio waendeshaji wa Mashindano ya BSS, Ritha Paulsen na kushoto ni Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Azikiwe, Hamis Saleh.

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Stephen Adili (kushoto) akimzungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi Mshindi wa BSS 2021 (Bongo Star Search), Yohana Braison Mwayinga, kitita cha shilingi milioni kumi (10,000,000/-) ikiwa ni zawadi ya mshindi wa kwanza, iliyofanyika leo kwenye tawi la Benki ya CRDB la Azikiwe, jijini Dar es salaam. kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya BenchMark ambao ndio waendeshaji wa Mashindano ya BSS, Ritha Paulsen

Mshindi wa BSS 2021 (Bongo Star Search), Yohana Braison Mwayinga akizungumza.

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi (Head of Consumer Banking), Stephen Adili (kushoto) pamoja na Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Azikiwe, Hamis Saleh (kulia) wakifurahia jambo baada ya kukabidi zawadi kwa washindi wa BSS 2021, Yohana Braison Mwayinga (mshindi wa kwanza), Andrew Charles Magalata (mshindi wa pili), Suleiya Abdi Abdillah (msindi wa tatu) wakiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya BenchMark ambao ndio waendeshaji wa Mashindano ya BSS, Ritha Paulsen. hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo kwenye tawi la Benki ya CRDB la Azikiwe, jijini Dar es salaam.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...