Mwenyekiti wa Clouds Media Group Joseph Kusaga (kushoto) akifanya mahojiano na Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania PLC, Sitholizwe Mdlalose kuhusu mipango-mkakati ya Vodacom kwa mwaka huu wa 2022 wakati Mkurugenzi huyo alipotembelea ofisi za Clouds Media na kupata fursa ya kujitambulisha kwa wafanyakazi chombo hicho.

Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania PLC, Sitholizwe Mdlalose akiwa kwenye chumba cha habari cha ITV na kufanya mahojiano wakati wa ziara ya Mkurugenzi huyo kwenye ofisi za IPP Media na kupata fursa ya kujitambulisha kwa wafanyakazi vyombo hivyo.
 Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania PLC, Sitholizwe Mdlalose (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Ltd, Bakari Machumu (kushoto)  Mkurugenzi huyo alipotembelea kwenye za Mwananchi  na kupata fursa ya kujitambulisha kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo. Katikati ni  Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC , Rosalynn Mworia.

Meneja Matangazo EATV, Lidya Igarabuza (kushoto) akifanya mahojiano na Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania PLC, Sitholizwe Mdlalose kuhusu mipango-mkakati ya Vodacom kwa mwaka huu wa 2022 wakati wa ziara ya Mkurugenzi huyo mpya wa Vodacom kutembelea ofisi za IPP Media ambapo EATV/Radio ni mojawapo.

Mhariri Mkuu wa Gazeti la The Guardian, Wallace Maugo (kulia) akielezea namna ya uendeshaji wa kila siku wa gazeti hilo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Sitholizwe Mdlalose (wa tatu kulia) na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC , Rosalynn Mworia (kushoto)

Mwenyekiti wa Clouds Media Group Joseph Kusaga (katikati) akimkaribisha Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania PLC, Sitholizwe Mdlalose kwenye kipindi cha XXL Clouds Fm kinachoongozwa na Adam Mchomvu (kulia)




 
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Sitholizwe Mdlalose (wapili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa ITV/Radio One na Capital Tv/Capital Radio, Joyce Mhavile (wa pili kulia), Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia (kulia) na Mkurugenzi wa Masoko wa ITV/Radio One na Capital Tv, Joyce Luhanga, mara baada ya Mkurugenzi mpya wa Vodacom kutembelea ofisi za IPP Media na kupata fursa ya kujionea utendaji kazi pamoja na kujitambulisha kwa wafanyakazi wa vyombo hivyo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...