Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mb, (katikati) akijibu hoja mbalimbali za Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi hao wa Wabunge yanayoendelea katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022, kushoto ni Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Zungu

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Zungu (Mb), akiongoza semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar,

Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa akiwasilisha mada kuhusu uzoefu, Changamoto na mbinu za uendeshaji bora wa vikao vya Bunge katika Bunge la Vyama vingi vya siasa katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022, katika ni Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) na Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Zungu


Spika Mstaafu, Mhe. Anne Makinda akidadisi mada kuhusu uzoefu, Changamoto na mbinu za uendeshaji bora wa vikao vya Bunge katika Bunge la Vyama vingi vya siasa iliyowasilishwa na Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar

Spika Mstaafu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Pandu Kificho akidadisi mada kuhusu uzoefu, Changamoto na mbinu za uendeshaji bora wa vikao vya Bunge katika Bunge la Vyama vingi vya siasa iliyowasilishwa na Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiwasilisha mada kuhusu uzoefu na changamoto za uratibu wa Shughuli za Bunge na Shughuli za Serikali katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar,

Mwenyekiti wa Bunge, Mhe. David Kihenzile akichangia jambo wakati wa semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Dkt. Eliazer Feleshi (kulia) pamoja na Waziri wa Nchi, ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Balozi Mhe. Dkt. Pindi Chana wakishiriki katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...