Na Amiri Kilagalila,Njombe

Katibu wa baraza la walei kanisa la Roman Katoliki kigango cha Parokia ya Makambako jimbo la Njombe mashariki Dickson Myamba (48) amekutwa ameuawa kwa kukatwa katwa na mapanga katika duka lililopo ndani ya kanisa hilo. 

Waumini wa kanisa katoliki Parokia ya Makambako mkoani Njombe wamejikuta katika kiiza kinene na sintofahamu baada ya usiku wa februari 7 kukuta mwili wa Nickson Muyamba aliyekuwa katibu wa baraza la walei kigango cha Makambako ndani ya duka la vitabu vya kiimani akiwa amekatwa na kitu chenye ncha kali na kisha kutenganishwa mwili wake vipande viwili.

Katika misa ya mazishi iliyofanyika katika kanisa la mtakatifu bikira Maria mama wa neema parokia ya Makambako  Padre Jordan Mwajombe ambaye ni Dekanusi wa Makambako amesema mauaji hayo ya kikatili ,hayaja fanywa kwa mpango wa mungu  na kwamba yamelitia doa kanisa katoliki kwa kutendeka katika eneo la kanisa na kwamba kanisa linakwenda kutenga siku 9 kwa ajili ya kufanya maombi maalumu ya marehemu na kuwafichua wahusika.

"Ndugu zangu kuna makosa mengine hata shetani anaweza akayakataa,kwamba mimi sikumtuma huyu alyefanya haya afanye hili "alisema Padre Jordan Mwajombe ambaye ni paroko wa parokia ya Kifumbwe

Serikali nayo imeshiriki misa na mazishi ya mtumishi huyo wa kanisa ambaye amepewa nafasi ya upendeleo ya kuzikwa katika viunga vya kanisa kwakuwa ameuawa akiwa kanisani  akiendelea na majukumu yake ,Ambapo mkuu wa wilaya ya Njombe Kissa Gwakisa Kasongwa kwaniaba ya mkuu wa mkoa akalaani vikali mauaji hayo na kisha kueleza  hatua ambazo zimeanza kuchukuliwa kubaini wahusika wa mauaji ili kuwafikisha mahakamani.

Nao baadhi ya waumini wa parokia hiyo akiwemo Rafaela Sanga wamemuelezea marehemu enzi za uhai wake huku nao madiwani wa baraza la Makambako  wakieleza hatua wanazokwenda kuchukua ili kuelimisha wananchi kwa lengo la kudhibiti mauaji.

Licha mauaji hayo kutekelezwa usiku wa kuamkia februari 8 lakini hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusika  Na Tukio Hilo.

Aidha jeshi la polisi mkoa wa Njombe linaendelea na uchunguzi juu ya mauaji hayo.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...