NA Abel Paul wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ACP JUSTINE MASEJO amesema tarehe Tarehe 01.03.2022 muda wa 06:30 mchana huko maeneo ya Ngaramtoni wilaya ya Arumeru na Mkoa wa Arusha askari wakiwa doria walifanikiwa kumkamata ELIA MBWAMBO (45) mkazi wa Ngaramtoni akiwa anasafirisha Dawa za kulevya yadhaniwayo kuwa ni mirungi yenye uzito wa 187kg.

Kamanda Masejo amesema kuwa Mtuhumiwa huyo alikamatwa akiwa anasafirisha madawa hayo maeneo ya Ngaramtoni kwa kutumia gari lenye namba za usajili T.793 CUY aina Varian.

Amesema kuwa Uchunguzi wa awali umebaini kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa akijihusisha na biashara hiyo haramu ya usafirishaji wa madawa ya kulevya katika maeneo mbalimbali jijini Arusha.ACP MASEJO

Ameendelea kusema kuwa mara baada ya pelelezi kukamilika jalada litapelekwa ofisi ya taifa ya mashtaka kwa ajili ya kulitolea maamuzi kisheria.

ACP Masejo ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwa Jeshi la Polisi ili kutokomeza kabisa uhalifu ndani ya mkoa wetu. Pia niwatake baadhi ya watu wachache wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya pamoja na matumizi ya madawa ya kulevya kuacha mara moja tabia hiyo kwani hatua kali za kisheria zitaendelea kuchukuliwa dhidi.







 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...