![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi_NMEv6Ke2oRx94mpDgpDlUGKYwcGnNNJbVAfLkP-lqJhEK3t9xfzIBtqhUHC3e-Jw25rWYj-JkMc7BYvhO7hWWk5FKp4ATMaMl6alnlwchpQsq0yROjQn6MJ0U9VXT42nRKdk0_o1qM5NjdnkiMYnYXtCTPZXWDN6bTN5izWZzZpRI9dktBo/w640-h462/1-104-2048x1477.jpg)
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation, Rosalynn Mworia akimsikiliza mkunga kutoka mkoa wa Shinyanga, Flora Kajumla baada ya kumkabidhi tuzo katika sekta ya afya kwenye tuzo za Kitchen Party Gala 2022 (Mwanamke wa Shoka) zilizoandaliwa na EFM. Asasi ya Vodacom Tanzania Foundation kupitia mradi wake wa M-Mama inawasaidia wanawake wajawazito mkoani humo kutumia simu zao za mkononi kuunganishwa na huduma ya dharura ili kuokoa maisha yao na ya mtoto kwa kupatiwa usafiri pindi wanapopatwa na uchungu pingamizi.
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2022/03/3-73-scaled.jpg)
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation, Rosalynn Mworia (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Biashara Vodacom Tanzania Plc, Linda Riwa (kulia) na Mkurugenzi wa Fedha Vodacom Tanzania Plc,Hilda Bujiku wakati wa hafla ya utoaji tuzo za Kitchen Party Gala 2022 (Mwanamke wa Shoka) zilizoandaliwa na EFM. Asasi ya Vodacom Tanzania Foundation kupitia mradi wake wa M-Mama inawasaidia wanawake wajawazito mkoani humo kutumia simu zao za mkononi kuunganishwa na huduma ya dharura ili kuokoa maisha yao na ya mtoto kwa kupatiwa usafiri pindi wanapopatwa na uchungu pingamizi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...