Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika kumbukizi ya miaka 100 ya  kuzaliwa Hayati baba  wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambayo inatarajiwa kufanyika katika chuo cha Uongozi cha mwalimu Nyerere  kilichoko Kibaha mkoani Pwani. 

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Pwani ,Mkuu wa mkoa huo Abubakari Kunenge amesema sambamba na kumbukizi  hiyo ya baba wa Taifa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Pwani kimeandaa mdahalo .

Mdahalo huo una lengo la kutafakuri maisha ya mwalimu Nyerere ambao utafanyika April 9 mwaka huu katika chuo hicho.

Kunenge amebainisha,kila april 13 huwa kumbukizi ya kuzaliwa safari hii ,kumbukizi hii itatimiza miaka 100 ya mwl.Nyerere.

Hayati Baba wa Taifa  Mwalimu  Julias Nyerere alizaliwa April 13 , mwaka 1922  kijijini Butiama mkoa wa Mara, na amefariki dunia mwezi October  mwaka 1999.


 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...