Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
RAIS
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa
 mgeni Rasmi katika kumbukizi ya miaka 100 ya  kuzaliwa Hayati baba  wa 
Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambayo inatarajiwa kufanyika katika chuo 
cha Uongozi cha mwalimu Nyerere  kilichoko Kibaha mkoani Pwani. 
Akizungumza
 na waandishi wa habari mkoani Pwani ,Mkuu wa mkoa huo Abubakari Kunenge
 amesema sambamba na kumbukizi  hiyo ya baba wa Taifa Chama cha 
Mapinduzi mkoa wa Pwani kimeandaa mdahalo .
Mdahalo huo una lengo la kutafakuri maisha ya mwalimu Nyerere ambao utafanyika April 9 mwaka huu katika chuo hicho.
Kunenge amebainisha,kila april 13 huwa kumbukizi ya kuzaliwa safari hii ,kumbukizi hii itatimiza miaka 100 ya mwl.Nyerere.
Hayati
 Baba wa Taifa  Mwalimu  Julias Nyerere alizaliwa April 13 , mwaka 1922 
 kijijini Butiama mkoa wa Mara, na amefariki dunia mwezi October  mwaka 
1999.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...