Njombe

Mahakama ya wilaya ya Makete mkoani Njombe imemsomea shtaka la ulawiti ndugu,Bahati Langson Sanga (36) mkazi wa kijiji cha Ihanga kata ya Ukwama anayetuhumiwa kwa kosa la kumlawiti mtoto.

Imeelezwa kuwa mnamo tarehe 17 Aprili 2022  katika kijiji cha Ihanga  mshtakiwa alitenda kosa hilo la kumlawiti mtoto  kinyume na kifungu cha 154 (1)a  ya kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo 2019.

Hata hivyo amesomewa shtaka lake na kukanusha kutenda kosa hilo.

Shauri hilo limeongozwa na hakimu mkazi mfawidhi wilaya ya Makete Mh.Ivan Msaki pamoja na mwendesha mashtaka ambaye ni Inspecta wa jeshi la Polisi  Benstard Mwoshe.
 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...