Benki ya NMB imetenga Sh. bilioni moja kwaajili ya kuwasaidia wabunifu wachanga waweze kuimarika na kuzifanya bunifu zao kuwa bora na zenye manufaa kwa uchumi wa Taifa kwa ujumla.

Hayo yameelezwa na Meneja Idara ya Utafiti wa Benki ya NMB, Prochest Kachenje alipokuwa anamuelezea Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Omary Juma Kipanga alipotembelea banda la NMB wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Tafiti na Ubunifu ya chuo kikuu cha Dar es Salaam.

“NMB imetenga shilingi bilioni moja kwaajili ya kuwasaidia wabunifu wanaochipukia kuweza kuziweka bunifu zao katika utekelezaji ili waweze kunufaika”

“Mwaka jana tulizindua mfumo maalumu wa NMB Sandbox Environment ambapo wabunifu wa suluhishi mbalimbali za kifedha wanaweza kufanya majaribio ya bunifu zao na kwa zitakazo fuzu, tutashirikiana nao,” aliongezea Prochest.

Lakini pia, Prochest alisema kuwa kiasi hiki cha fedha sio mkopo bali ni fedha iliyotengwa kwa dhumuni ya kusaidia wabunifu hawa na hawatawajibika kuirejesha.

Alitumia pia fursa hiyo kuwakaribisha wanachuo na Vijana wabunifu kuishirikisha Benki ya NMB juu ya bunifu zao ili kuwasaidia kupata fedha za kuboresha zaidi.



Meneja wa utafiti wa Benki ya NMB, Prochest Kachenje akizungumza na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Omary Juma Kipanga alipotembelea banda la NMB wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Tafiti na Ubunifu – Chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Maafisa wa benki ya NMB kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Tafiti na Ubunifu – Chuo kikuu cha Dar es Salaam.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...