Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Daniel Chongolo amemtaka mbunge wa Jimbo la Itilima Njalu Silanga kuwawezesha wakulima wa Jimbo Hilo kuhakikisha Kila tarafa wanapata Mashine ya kukamua mafuta ya alizeti Ili kuongeza thamani ya zao hilo ambapo kwa Mkoa wa Simiyu, Itilima inaongoza kwa uzalishaji wa alizeti.


"Najua Mbunge wenu ana wajibu wa kuwasaidia mashine za kuchuja mafuta ya alizeti, wasaidie wananchi Hawa wapate mashine za kuchuja mafuta ya alizeti angalau kwa mashine moja kwa Kila tarafa na hili litawasaidia sana kuongeza thamani ya zao hili."

Katibu Mkuu ameongeza kuwa kitendo Cha kufunga mashine, wakulima wataanza kuuza mafuta badala ya kuuza alizeti zenyewe, ambapo kwa sasa mafuta ya alizeti ndio mafuta bora na ghali zaidi, hivyo wananchi watapata fedha za kutosha tofauti na sasa.

Chongolo ameyasema hayo leo tarehe 2 Juni, 2022 alipowasili Wilayani Itilima Mkoa wa Simiyu wakati akiendelea na ziara yake yenye lengo la kukahamasisha uhai wa Chama ngazi za mashina na Kukagua utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.













Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...