WAKAZI
zaidi ya 3,500 wa Mitaa ya Mwanalugali A na B ,kata ya Tumbi ,wilaya ya
Kibaha Mkoani Pwani wanatarajia kuondokana na kero ya kutembea umbali
wa kilometa kumi kufuata huduma za afya kituo cha afya Mkoani na
hospital ya Rufaa ya Tumbi baada ya ujenzi wa Zahanati ya Mwanalugali
kukamilika mwezi septemba mwaka huu.
Ujenzi huo Hadi Sasa umefikia asilimia 70 ambapo umeanza mwezi march mwaka huu.
Akitembelea
mradi wa miundombinu ulioibuliwa na wananchi na kufadhiliwa na Mfuko wa
Maendeleo ya jamii(TASAF) , Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge
alitoa agizo kwa mganga Mkuu wa mkoa kuhakikisha wanaandaa wataalamu na
watendaji wa afya mapema ili mradi ukianza wawepo tayari.
Agizo jingine Ni kuwepo kwa vifaa tiba ili huduma zianze Mara moja baada ya ukamilishaji wa mradi huo.
Pia
Kunenge amemuagiza, mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, na
wataalamu wake kupima na kuandaa mchoro na Hati kwa eneo hilo ili
kuondoa changamoto za migogoro ya ardhi isije kujitokeza baadae .
Pamoja
na hayo ,ameitaka Mamlaka ya maji na usafi wa Mazingira Dar es Salaam
(DAWASA) na Shirika la Umeme ( TANESCO) kuweka Mazingira mazuri ya
upatikanaji wa huduma hizo wakati wa utoaji huduma Sambamba na TARURA
ihakikishe inachonga barabara zote zinazoelekea katika Zahanati ya
Mwanalugali ili kuondoa usumbufu.
Awali
mkazi wa Mwanalugali, Frida Mvalla ,alieleza mradi huo utakuwa mkombozi
kwao kwani walikuwa wakipata shida hasa kwa wajawazito na Watoto pamoja
na kuhangaika endapo kunatokea wagonjwa nyakati za usiku.
Nae
Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Mji wa Kibaha,Anita Lioka alisema ,
wananchi wameibua mradi huo na TASAF imefadhili ambapo utagharimu kiasi
cha sh.milioni 113.6.
Alitaja changamoto za mradi kuwa ulisimama wiki mbili kutokana na mvua na ,ongezeko la vifaa .
Licha ya hayo ,wanaomba kuongezwa jengo la kujifungulia ili kusaidia wakinamama na watoto .
"Tunamshukuru
Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha jamii kupitia fedha za TASAF na
kusaidia kaya maskini,Kwakuwa itasaidia kuwaondolea kero wananchi hawa",
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...