Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amesema kuwa Serikali itaendelea kutatua changamoto za migogoro ya mipaka kati ya hifadhi na wananchi ili wananchi wajue maeneo ya vijiji na kuheshimu mipaka ya Hifadhi.
Ameyasema hayo leo Juni 28, 2022 Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Nkasi, Mhe. Aida Joseph Khenani, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kupitia mipaka ya Hifadhi na Makazi ya Wananchi Wilayani Nkasi.
Amefafanua kuwa Serikali imeweka vigingi 111 kati ya 322 vinavyohitajika katika Pori la Akiba Lwafi Wilayani Nkasi ili kuainisha mipaka ya hifadhi hiyo.
Aidha, amesema Serikali inaendelea na jitihada za kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kutambua na kuheshimu mipaka ya Hifadhi.
Kuhusu migogoro ya mipaka kati ya Vijiji vya Vilima Vitatu, Mwada na Ngolee na Hifadhi ya Tarangire Wilayani Babati, Mhe. Masanja amefafanua kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi itatuma wataalam kwenda kufafanua au kutafsiri mipaka ili wananchi wajue maeneo ya vijiji na kuheshimu mipaka ya hifadhi.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...