MCHEZO wa golf maarufu kama DIPLOMATIC GOLF TOURNAMENT unatarajiwa kufanyika kwa mara ya nne kuanzia tarehe 24 na 25 Septemba katika viwanja vya Kiligolf vilivyopo USA RIVER jijini Arusha Tanzania.

Mchezo huu wa Diplomatic Golf unaandaliwa na taasisi binafsi ya Songea Mississippi Foundation(SOMI) kwa kushirikiana na Kiligolf  kwa lengo la kusaidia watoto wenye mazingira magumu songea.

Diplomatic golf 2022 utahusisha wachezaji wa golf kutoka ndani na nje ya nchi lengo likiwa ni kutengeneza mahusiano na connection baina ya wachezaji na watazamaji.

Mwaka huu tunatarajia kuwa na wachezaji zaidi ya 200 ambapo kiingilio kitakuwa kama ifuatavyo:

Tarehe 24 September - 18 holes (Mashimo 18)

     20usd sawa na 45,000/=Tzs kwa mchezaji mmoja

     100usd sawa na 230,000/=Tzs kwa kundi la wachezaji wanne

Kwa Wachezaji watakaotaka kucheza siku zote mbili kiingilio kitakuwa kama ifuatavyo:

Tarehe 24 na 25 Septemba - 36 holes (Mashimo 36)

     30usd sawa na 70,000/= kwa mchezaji mmoja

     200usd sawa na 460,000/= kwa kundi la wachezaji wanne

Kwa kupitia lengo la mchezo huu tunawaalika wachezaji wote wa Golf kushiriki mchezo huu.

Pia nafasi za udhamini ziko wazi tunawalika wadhamini waje kushirikiana nasi kufanikisha hii event huku tukitoa tabasamu kwa watoto wanaohitaji.

 Kwa mawasiliano zaidi 0719353633 Waandaaji












Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...