Na Farida Mangube, Morogoro
SERIKALI
ya awamu ya sita chini ya Wizara ya Maji kupitia Mamlaka ya Maji Safi
na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA),imeanza kutekeleza mradi
mkubwa wa maji wenye thamani ya Sh bilioni 185 kwenye Manispaa ya
Morogoro.
Fedha hizo
zinatokana na ufadhili kutoka Shirika la Maendeleo la Ufarasa (AFD),
ambao unalenga kuboresha Bwawa la Mindu na mundombinu ukiwemo ujenzi a
mtambo mpya wa kutibu maji eneo la Mafiga.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Morogoro
(MORUWASA), Mhandisi Tamimu Katakweba alisema hayo jana kwenye
taarifa yake mbele ya Kiongozi wa mbio Kitaifa 2022 , Sahil Geraruma.
Mwenge
wa Uhuru uliweka jiwe la msingi kwenye mradi wa uboreshaji wa huduma
ya maji kwa wananchi wa Mitaa ya Kasanga na Mgaza ambao idadi yao
imeongezeka kutoka 3,918 mwaka 2014 na sasa kukadiriwa kufikia wakazi
wapatao 10,000
Mhandisi
Katakweba alisema mradi huo wa kimkakati unatarajia kukamilika mwaka
2025 ambao utazalisha maji lita milioni 89 ukilinganisha na mahitaji ya
lita 86 kwa siku mwaka 2025.
Alisema
umejikita kuboresha Bwawa la Mindu kwa kunyanyua kuta na kuondoa tope
, ujenzi wa mtambo mpya wa kutibu maji utakaojengwa eneo la Mafiga,
ujenzi wa mabirika ya kuhifadhi maji yenye uwezo wa kuhifadhi lita
milioni 11 kwa wakati mmoja na utafutaji wa vyanzo vya maji mbadala
ukiwemo maji ya chini ya ardhi.
Mhandisi
Katakweba alisema kwa sasa mahitaji ya maji kwa Manispaa hiyo ni lita
milioni 73 kwa siku ulilinganisha na lita milioni 35 zinazozalishwa kwa
sasa .
Kwa upande wa
mradi wa uboreshaji wa huduma ya maji Kasanga ulibuniwa na Manispaa ya
Morogoro mwaka 2014 ulikuwa na lengo la kuhudumia wakazi 3,918 wa mtaa
wa Kasanga na Mgaza na ulikabidhiwa kwa mamlaka 2017 kwa ajili ya
uendeshaji.
Alisema mradi
huo ulitekelezwa na fedha za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na
Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Covid -19 ambapo kiasi cha Sh milioni
590.9 zilitolewa na Serikali ,wakati Sh milioni 25.3 zilizotolewa na
Moruwasa zilitumika kuboresha mradi huo ili wananchi wa mitaa ya Kasanga
na Mgaza wapatao waweze kupata huduma bora ya maji.
Alisema
mradi huo ulikabidhiwa kwa Mamlaka hiyo mamlaka 2017 kwa ajili ya
uendeshaji na baada ya maboresho makubwa utapunguza tatizo la mgao wa
maji kwa wananchi wa Kata ya Mindu kutoka siku 14 za awali na sasa
watapata maji kila baada ya siku moja.
Hivyo
alisema mradi huo baada ya uboreshaji mkubwa utakuwa na uwezo wa
kusambaza maji lita 700,000 kwa siku huku mahitaji yakiwa ni lita
941,500.
“ Mradi huu
mwaka huo ulipokelewa ukiwa na changamoto mbalimbali ikiwemo, usanifu
ulizingatia kutoa huduma kupitia vizimba badala ya kuunganisha maji
kwenye nyumba za wananchi kama sera ya maji ya mwaka 2002 inavyoelekeza”
alisema Mhandisi Katakweba
Pia
alisema serikali kupitia Mamlaka hiyo imekalisha miradi ya maji ya
matokeo ya haraka kwenye maeneo ya Bigwa-Bohmela, Mambogo-Kihonda,
Mkundi – Lukobe, Mindu, Mgadu, Kauzeni na Bong’ola ambapo Sh Bilioni 12
na itaongeza lita milioni 17 kwenye mfumo hivyo kuongeza uzalishaji toka
asilimia 48 za sasa na kufikia asilimia 71 kufikia Juni 2023.
Kwa
upande wake Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Geraruma
licha ya kupongeza hatua hizo aliwataka wananchi wa Manispaa hiyo
wakiwemo wa kata ya Mindu kupanda miti kwenye vyanzo vya maji na kuacha
kufanya shughuli za kijamii kweye vyanzo hivyo.
“Tusilime
kwenye vyanzo vya maji tusifuge kwenye vyanzo vya maji na shughuli
nyingine zote tusifanye kwenye vyanzo vya maji cha zaidi ndugu zangu
wana Mindu tutunze vyazo vya maji au kupanda miti rafiki kwenye vyanzo
vya maji” alisema Geraruma
Kwa
upande wake Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Abdulaziz Abood
alimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Moruwasa kwa ushirikiano mkubwa
anaoutoa kwa ofisi ya mbunge katika kuhakikisha wananchi wa jimbo hilo
wanapata huduma ya maji safi na salama.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...