Na Jane Edward, Arusha

Takribani wakandarasi 18 waliosaini mikataba  ya kutengeneza miundo mbinu ya barabara na madaraja, wametakiwa kufanya kazi kwa weledi  kwa kuzingatia muda ambapo kwa wale watakaoenda kinyume na taratibu walizojiwekea kushughulikiwa.

Hayo yamesemwa jijini Arusha na Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongela wakati wa zoezi la utiaji Saini kwa wakandarasi wa barabara na madaraja.

Mongela amesema Mikataba hiyo  ina thamani ya sh,bilioni 4 kati ya Wakala wa barabara vijijini na Mijini ( TARURA) na wakandarasi 18 ,huku fedha hizo zikiwa ni fedha za nyongeza zilizotokana na tozo.

" wakandarasi mnatakiwa kufanya kazi kwa  kufuata miongozo iliyopo kwenye mikataba hiyo , kwa kutekeleza mradi kwa viwango na kuepuka  ucheleweshaji na kutokidhi ubora wa mradi"Alisema Mongela

Meneja wa TARURA Mkoa wa Arusha mhandisi  Laynas Sanya alisema kwa mwaka wa fedha 2022/2023 walipatiwa jumla ya fedha za matengenezo ya barabara  zaidi ya  bilioni 18 kwa awamu ya pili na katika awamu ya kwanza mikataba 34 ilisainiwa yenye  thamani ya bilioni 14.

Aidha  awamu ya pili ya utiaji saini  jumla ya mikataba 18 yenye thamani ya zaidi ya sh,bilioni 4 imesainiwa na wakandarasi mbalimbali wazawa watakaotekeleza miradi ya miezi sita kwa kiwango na ubora unaotakiwa.

"Mikataba hii tumesaini ikiwa ni kufuata mwongozo wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ambaye alielekeza mikataba yote isainiwe hadharani bila usiri"Alisema meneja

Akifafanua zaidi amesema  wakati wa utekelezaji wa miradi ya barabara mwongozo wa serikali unawataka pia kuweka taa za  barabarani jambo ambalo alisisitiza  wameanza kulitekeleza.

Hata hivyo alisisitiza kuwa Tarura itahakikisha inawasimamia wakandarasi hao ili miradi hiyo inayotengenezwa iweze  kukamilika kwa wakati .

Mkuu wa Mkoa wa Arusha akigawa mikata iliyosainiwa na wakandarasi Mkoa wa Arusha.

 Kulia aliyevaa miwani ni meneja wa TARURA Mkoa wa Arusha Laynas Sanya akishuhudia zoezi la utiaji saini kwa wakandarasi hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...