Na mwandishi wetu, Arusha
Tatizo  la kumaliza  uwepo wa sumu kuvu katika zao la muhogo limepatiwa ufumbuzi na  Taasisi ya Uhandisi na Usanifu  Mitambo Tanzania (TEMDO)  mara baada ya kuwabunia wakulima wa zao hiyo mtambo utakao wasaidia  kuchakata  zao hilo   mara tu baada ya   kuvunwa .

 Hayo yamebainishwa na Ofisa wa kitengo cha Mawasiliano na Masoko Dkt. Sigisbert Mmasi kutoka Taasisi ya ubunifu na Usanifu mitambi Tanzania (TEMDO) wakati akiongea katika  maonyesho ya 17 ya SIDO Kanda ya kaskazini yanayofanyika katika viwanja vya makumbusho vilivyopo ndani ya halmashauri ya jiji la Arusha mkoani Arusha  ambapo alisema kuwa mashine hiyo itamkomboa sana mkulima wa zao la muogo

 Alisema kuwa Mtambo huu utakuwa mkombozi  kwa wakulima kwakuwa   muhogo ukivunwa unatakiwa  uchakatwe mapema maana ukikaa sana unaweza ukaharibika ,ukatengeneza sumu kuvu ambayo ni  Kuvu/ukungu/fangasi hushambulia mazao mbalimbali ya chakula, ambapo kawaida kuvu hupatikana kwenye udongo wakati wote katika hali ya vumbi  au muhogo huo  ukaharibika ukawa haufai tena kwa matumizi ya  binadamu

 Alibainisha kuwa  temdo kila mwaka wanakuja na kitu kipya ambacho kitamsaidia mkulima  katika kazi  zake pamoja na kutatua matatizo  katika kilimo anachofanya  ,na kwa mwaka huu wameamua kumletea mkulima mtambo huo ambao utamsaidia mkulima kuokoa mazao yake ambayo yalikuwa yakiaribika   kutokana na kukosa soko

 Alisema kuwa mtambo huo  unauwezo wa kuchakata zao la muhogo takribani tani 12  na wenyewe unakuwa na tani elfu 12000 za muhogo ambapo ukichakata unapata unga takribani  tani  tatu.

“mtambo huu ni wa kisasa na unamsaidia mkulima kwa sababu unauwezo wa kuvuna muhogo siku hiyo hiyo na  kuchakata siku hiyo hiyo  ,na niwaambie ukishavuna muhogo wako unaumenya unaingiza kwenye mashine  unatengenezwa uji baada ya  apo  unawekwa kwenye draya  ambayo inasaidia kukausha ule unga wa muhogo siku hiyo hiyo kwa iyo unapata unga siku hiyo hiyo ,na unaweza kupeleka kwa walaji siku hiyo hiyo“alibainisha Mmasi

Alisema kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ya kutokuwa na mvua  kwa kipindi kirefu  mtambo huo utasaidia kuokoa kile chakula ambacho kilikuwa kinapotea kwa kuoza bure  kutokana na kukaa mda mrefu bila kuchakatwa .




Afisa wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Dkt. Sigisbert Mmasi kutoka Taasisi ya ubunifu na Usanifu mitambi Tanzania (TEMDO)akiongea na baadhi ya wananchi waliotembelea  banda lao lililopo katika maonyesho ya 17 ya SIDO Kanda ya kaskazini yanayofanyika katika viwanja vya makumbusho vilivyopo ndani ya halmashauri ya jiji la Arusha mkoani Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...