Wizara
ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya
pamoja na Sekta Binafsi ya Tanzania imeandaa Kongamano la Biashara kati
ya Tanzania na Nchi za Umoja wa Ulaya linalotarajiwa kufanyika kuanzia
tarehe 23 hadi 24 Februari, 2023 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius
Nyerere (Julius Nyerere International Conference Centre) uliopo jijini
Dar es Salaam.
Kongamano hilo linatarajiwa kujumuisha zaidi ya
washiriki 600 kutoka nchi za Umoja wa Ulaya na Tanzania linalenga
kuwaunganisha washiriki hao ili kuwawezesha kubadilishana uzoefu,
kushirikiana na watoa maamuzi na kukutana na wawekezaji wanaofaa pamoja
na kujenga uelewa kuhusu fursa za uwekezaji zilizopo kwa sekta ya umma
na binafsi ambapo, Hati za Makubaliano mbalimbali ya Uwekezaji baina ya
Tanzania na Nchi za Umoja wa Ulaya zitatiwa saini.
Kongamano
hilo linatarajiwa kuzinduliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango, akimwakilisha
Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na litafungwa rasmi na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,
Mheshimiwa Dkt. Hussein Mwinyi ambaye atashuhudia utiaji saini wa
mikataba ya fedha na hati za makubaliano.
Aidha, Kongamano hili
litahudhuriwa na Mawaziri nane (8) kutoka Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na
Mabalozi sita (6) wa Tanzania katika nchi za Umoja wa Ulaya ambao
watashiriki katika vikao vya majadiliano kati ya Serikali na Biashara.
Hivyo
ninatarajia kuona Kongamano hili la Biashara la kwanza kuwa fursa ya
kuvutia wawekezaji, teknolojia na utalaamu katika nchi yetu na kuvutia
biashara na uwekezaji kutoka duniani kote katika sekta za nishati,
madini na kilimo endelevu. Hivyo tunatarajia hati za makubaliano
zitakazotiwa saini zitaendeleza na kukuza biashara kati ya Tanzania na
Umoja wa Ulaya, zitaongeza ajira kwa vijana na zitachangia katika ukuaji
wa uchumi wa nchi yetu
Aidha, Wafanyabiashara na wawekezaji
kutoka Tanzania mtumie fursa hii vizuri kuendeleza na kukuza biashara
yenu kwa kujifunza mbinu mpya za kibiashara, kupata wabia na masoko ya
bidhaa zetu nje ya nchi.Waziri
wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji( katikati)
akizungumza kwenye mkutano wa waandishi wa habari kuhusu kongamano la
uwekezaji la Umoja wa nchi za Ulaya(EU Tanzania business forum 2023)
linalotarajiwa kufanyika alhamisi na ijumaa wiki ijayo, linalolenga
kuwaunganisha wawekezaji wa nje na wafanyabiashara wa ndani ya ujumla
wao 600 kwa kubadilishana uzoefu na kushirkiana na watoa maamuzi.
Wengine kushoto ni Naibu mkuu wa shughuli za ubalozi kutoka ubalozi wa
Ufaransa nchini, Axel-David Guillon, Naibu Balozi wa EU nchini, Emilio
Rossetti, wapili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wizara ya Uwekezaji, Ally
Gugu na kulia ni Kinanasy Seif kutoka TPSF
Kinanasy Seif kutoka TPSF akizungumza na waandishi wa habari na wadau waliohudhuria kwenye mkutano huo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...