Katika kuimarisha uelewa wa matumizi ya bima kwa Jamii, Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) kwa kushirikiana na Kampuni pamoja na watoa huduma za bima wamezindua rasmi Kijiji cha Bima katika maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam, maarufu Sabasaba. Uzinduzi huo umefanyika tarehe 28 Juni 2024 kwa kuliambatana na shughuli mbalimbali za kihistoria na za kuvutia.

Tukio hilo lilihudhuriwa na watendaji wakuu (CEO’s) wa kampuni mbalimbali za bima chini ya Jumuiya ya Watoa Huduma za Bima Tanzania (ATI).

Uwepo wa wadau hao wa bima kwa katika tukio umeonesha dhamira ya dhati ya kuhakikisha huduma zinazotolewa kwa watanzania zinaendelea kuwa za viwango, sikivu na zenye manufaa kwa wote.

Aidha, Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania Kanda ya Mashariki, Bw. Zakaria Muyengi ambaye alimuwakilisha Kamishna wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware kuzindua rasmi Kijiji cha bima kwa kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi ameeleza kwamba TIRA imejipanga kuhakikisha elimu ya bima inawafikia watanzania wengi zaidi, kwa lengo la kuboresha ustawi na usalama wa kifedha na hali za wananchi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi kutoka Sekta ya Bima nchini 2024, Bw. Agustino Ndabala, ambaye pia ni Afisa Biashara wa Kampuni ya Bima ya Grandree Insurance Tanzania, alieleza jinsi Kijiji cha Bima kilivyopangiliwa. 

Alisema kuwa Kijiji cha Bima kimeanzishwa kwa lengo la kutoa elimu ya bima kwa umma, kuwajengea Watanzania uelewa wa kina kuhusu umuhimu wa bima katika maisha yao ya kila siku, na kuwahamasisha kutumia huduma za bima.

Kupitia maonesho haya, wananchi watapata fursa ya kukutana na wataalamu wa bima, kuuliza maswali, na kupata majibu yanayohusu bima kwa kina.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...