Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Hajjat Fatma Mwassa, wameungana na Maaskofu, Mapadri, Viongozi wa Kanisa Katoliki na waumini kushiriki Misa Takatifu ya mazishi ya Hayati Askofu Mkuu Novatus Rugambwa, Balozi wa Baba Mtakatifu.

Misa hiyo Takatifu imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora, Kardinali Protase Rugambwa, katika Kanisa Kuu Katoliki Jimbo la Bukoba, mkoani Kagera, leo tarehe 29 Septemba 2025.

Viongozi mbalimbali na wanafamilia walishiriki Misa hiyo, akiwemo Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Mhashamu Wolgang Pisa; Balozi wa Vatican nchini Tanzania, Askofu Mkuu Angelo Acattino; Askofu wa Jimbo Katoliki Bukoba, Mhashamu Jovitus Mwijage; pamoja na Mapadri, Watawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha, na waamini kutoka ndani na nje ya mkoa wa Kagera.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...