Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Japan kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Japan katika maendeleo ya rasilimali watu hususan kwenye sekta ya ujenzi.


Katika mazungumzo hayo, pande zote mbili zimejadili fursa za kuboresha ujuzi wa wataalam wa sekta ya ujenzi kupitia mafunzo, kubadilishana uzoefu na programu maalumu za kukuza uwezo. 

Aidha, Ujumbe wa Japan umeonesha utayari wa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha nguvu kazi ya Kitanzania inakuwa na weledi unaokidhi mahitaji ya soko la kimataifa.


Mazungumzo hayo yamefanyika leo Novemba 24, 2025 Jijini Dar es salaam ambapo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mohmoud Thabit na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Bi. Zuhura Yunus wamehudhuria mazungumzo hayo.






Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...