Pichani: Washambuliaji wa Timu ya EWURA (wenye jezi za bluu) wakishambulia timu pinzani wakati wa mchezo huo leo.

MOROGORO.

 Timu ya Mpira wa Wavu kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kung’ara katika mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMMUTA) baada ya kuichakaza timu ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa seti mbili mfululizo.

Katika mchezo huo uliochezwa leo mkoani Morogoro, EWURA ilipata pointi 25 katika seti zote mbili, huku NEMC ikijitahidi lakini ikibaki na pointi 23 kwenye seti ya kwanza na 17 katika seti ya pili.

Mchezo huo uliovuta hisia za mashabiki ulitawaliwa na kasi, nidhamu na uchezaji wa kimkakati kutoka kwa EWURA, ambao washambuliaji wao walionekana kuwa imara zaidi dhidi ya ngome ya NEMC.

Pichani: Washambuliaji wa Timu ya EWURA (wenye jezi za bluu) wakishambulia timu pinzani wakati wa mchezo huo leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...