Na. Mwandishi wetu - Rukwa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu amesema Serikali itaanzisha kitengo maalum cha huduma kitakachofanya kazi kwa saa 24 chenye jukumu la kupokea, kusikiliza na kufanyia kazi maoni, mapendekezo pamoja na kero za wananchi.

Kitengo hicho kitawezesha wananchi kuwasilisha changamoto zao moja kwa moja bila vikwazo vya kiurasimu na kusaidia Serikali kupata mrejesho wa haraka kwa ajili ya kuboresha sera na huduma.

Mhe. Sangu amebainisha hayo Disemba 23, 2025 Sumbawanga Mkoani Rukwa alipofanya kikao na wadau wa Mahusiano kutoka makundi ya Kijamii, Kisiasa, Kiuchumi na wawakilishi wa kundi la Vijana.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa mawasiliano na uwajibikaji kati ya Serikali na wananchi kwa ajili ya kuimarisha imani, mshikamano wa kitaifa na maendeleo jumuishi.

‎Aidha, amesema lengo la kikao ni kutambulisha shughuli za Ofisi yake na kutekekeza mkakati wa kuwafikia wadau wa mahusiano ili kujenga uelewa wa pamoja kwa maendeleo ya Taifa.

Kikao hicho kimeongozwa na Kauli mbiu isemayo "Mahusiano imara, Msingi wa Mshikamo wa Taifa"



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...