Dodoma, Desemba 17, 2025
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inapenda kuufahamisha umma kuwa Serikali ya Marekani imetangaza kuiweka Tanzania katika kundi la nchi zilizowekewa vikwazo visivyokamilika vya kuingia nchini Marekani (partial restrictions and entry limitation).
Tangazo la kuiweka Tanzania katika vikwazo hivyo limetangazwa na Rais wa Marekani, Mhe. Donald Trump kupitia mitandao yake rasmi ya kijamii mnamo Desemba 16, 2025.
Nchi nyingine ambazo zimewekwa katika utaratibu huo ni: 1. Angola, 2. Benin, 3. Cote d’Ivoire, 4. Gabon, 5. Gambia, 6. Malawi, 7. Mauritania, 8. Nigeria, 9. Senegal, 10. Zambia na 11. Zimbabwe.
Kwa mujibu wa Tangazo hilo, Uamuzi huo umetokana na baadhi ya Watanzania kutozingatia masharti ya viza za kuingia nchini Marekani na kupelekea zuwio hilo kufuatia taarifa ya Wakaazi waliopitiliza Muda (Overstay Report) iliyoonesha kuwa kuna kiwango kikubwa cha Raia wa Tanzania ambao wanakaa nchini Marekani kinyume cha Sheria kwa zaidi ya muda ulioruhusiwa na visa zao.
Taarifa hiyo ilionesha kuwa Tanzania imekuwa na kiwango kikubwa cha ukaaji wa zaidi ya muda kwa asilimia 8.3% kwa Visa zote za B-1/B-2 (Visa za biashara na utalii) na asilimia 13.97% kwa Visa za kundi la F, M na J (ambazo ni Visa za Wanafunzi, Mafunzo ya Ufundi, na programu za Kubadilishana yaani Exchange Programmes).
Kwa mujibu wa Taarifa hiyo, viwango hivyo vilitathminiwa kuwa vinazidi hali ya kawaida inayokubalika chini ya sera za uhamiaji za Marekani, na hivyo kupelekea Tanzania kujumuishwa katika kundi la Vizuizi hivyo vya Viza.
Kufuatia hali hiyo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kujadiliana na Serikali ya Marekani kupitia njia za kidiplomasia kati ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania na Wizara ya Nje ya Marekani ili kulitafutia ufumbuzi suala hilo.
Aidha, Serikali inawasihi Watanzania wote wanaosafiri kwenda nchini Marekani, kufuata kikamilifu masharti ya Viza hizo na kuepuka kuongeza muda wa kukaa kinyume cha sheria ya Viza hizo, jambo ambalo limepelekea Tanzania kuwekwa kwenye kizuizi hicho kusaidia jitihada za Wizara kuondoa Kizuwizi hicho.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali.
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inapenda kuufahamisha umma kuwa Serikali ya Marekani imetangaza kuiweka Tanzania katika kundi la nchi zilizowekewa vikwazo visivyokamilika vya kuingia nchini Marekani (partial restrictions and entry limitation).
Tangazo la kuiweka Tanzania katika vikwazo hivyo limetangazwa na Rais wa Marekani, Mhe. Donald Trump kupitia mitandao yake rasmi ya kijamii mnamo Desemba 16, 2025.
Nchi nyingine ambazo zimewekwa katika utaratibu huo ni: 1. Angola, 2. Benin, 3. Cote d’Ivoire, 4. Gabon, 5. Gambia, 6. Malawi, 7. Mauritania, 8. Nigeria, 9. Senegal, 10. Zambia na 11. Zimbabwe.
Kwa mujibu wa Tangazo hilo, Uamuzi huo umetokana na baadhi ya Watanzania kutozingatia masharti ya viza za kuingia nchini Marekani na kupelekea zuwio hilo kufuatia taarifa ya Wakaazi waliopitiliza Muda (Overstay Report) iliyoonesha kuwa kuna kiwango kikubwa cha Raia wa Tanzania ambao wanakaa nchini Marekani kinyume cha Sheria kwa zaidi ya muda ulioruhusiwa na visa zao.
Taarifa hiyo ilionesha kuwa Tanzania imekuwa na kiwango kikubwa cha ukaaji wa zaidi ya muda kwa asilimia 8.3% kwa Visa zote za B-1/B-2 (Visa za biashara na utalii) na asilimia 13.97% kwa Visa za kundi la F, M na J (ambazo ni Visa za Wanafunzi, Mafunzo ya Ufundi, na programu za Kubadilishana yaani Exchange Programmes).
Kwa mujibu wa Taarifa hiyo, viwango hivyo vilitathminiwa kuwa vinazidi hali ya kawaida inayokubalika chini ya sera za uhamiaji za Marekani, na hivyo kupelekea Tanzania kujumuishwa katika kundi la Vizuizi hivyo vya Viza.
Kufuatia hali hiyo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kujadiliana na Serikali ya Marekani kupitia njia za kidiplomasia kati ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania na Wizara ya Nje ya Marekani ili kulitafutia ufumbuzi suala hilo.
Aidha, Serikali inawasihi Watanzania wote wanaosafiri kwenda nchini Marekani, kufuata kikamilifu masharti ya Viza hizo na kuepuka kuongeza muda wa kukaa kinyume cha sheria ya Viza hizo, jambo ambalo limepelekea Tanzania kuwekwa kwenye kizuizi hicho kusaidia jitihada za Wizara kuondoa Kizuwizi hicho.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...