
Na Mwandishi Wetu
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Feb 23,2026 akiwa ameambatana na kamati ya usalama Mkoa, amesaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Askofu Mkuu mstaafu wa Jimbo la Dar es Salaam Mwadhama Cardinali Polycarp Pengo Kurasini Jijini humo.
Aidha Mkuu wa Mkoa pamoja na Kamati ya usalama alieleza masikitiko yake makubwa na kutoa rambirambi, kwa familia, Kanisa Katoliki na Taifa kwa ujumla ambapo amesema anamuomba mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahala pema peponi Amina.
Ifahamike kuwa maziko ya Mwadhama Cardinali Polycarp Pengo yanatarajiwa kufanyika Feb 28, 2026 Pugu Jijini Dar es Salaam kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...