Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Feb 23,2026 akiwa ameambatana na kamati ya usalama Mkoa, amesaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Askofu Mkuu mstaafu wa Jimbo la Dar es Salaam Mwadhama Cardinali Polycarp Pengo Kurasini Jijini humo.

Aidha Mkuu wa Mkoa pamoja na Kamati ya usalama alieleza masikitiko yake makubwa na kutoa rambirambi, kwa familia, Kanisa Katoliki na Taifa kwa ujumla ambapo amesema anamuomba mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahala pema peponi Amina.

Ifahamike kuwa maziko ya Mwadhama Cardinali Polycarp Pengo yanatarajiwa kufanyika Feb 28, 2026 Pugu Jijini Dar es Salaam kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam.



Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...