Na Pamela mollel,Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amepongezwa kwa juhudi zake za kuhamasisha wanawake kushiriki kikamilifu katika nyanja mbalimbali za maendeleo, hususan katika sekta za utalii na uhifadhi, hatua inayochangia kuongeza usawa wa kijinsia na kuwajengea wanawake ujasiri wa kushika nafasi za uongozi.
Pongezi hizo zimetolewa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Sekela Mwangota, ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini
Mwangota amesema uongozi wa Rais Samia umefungua fursa zaidi kwa wanawake kuamini uwezo wao, kujitokeza katika nafasi mbalimbali za uongozi na kushiriki kikamilifu katika maamuzi muhimu ya maendeleo ndani ya taasisi na jamii kwa ujumla.
Alitoa kauli hiyo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Machi 8, 2026 katika ukumbi wa Mafao House jijini Arusha, ambapo wanawake wa TANAPA waliungana kuadhimisha siku hiyo muhimu.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwangota alisema siku hiyo ni fursa ya kutambua mchango mkubwa wa wanawake katika maendeleo ya jamii,
Katika hafla hiyo iliyobeba ujumbe wa “Nguvu ya Mwanamke wa TANAPA, Fahari ya Uhifadhi na Utalii,” Mwangota alimkaribisha Mtaalamu wa Itifaki na Mwanadiplomasia Mwandamizi, Omary Kashera, kutoa mada kuhusu nafasi ya wanawake katika uongozi na maendeleo.
Kashera alisema kuwa Siku ya Wanawake Duniani ilianzishwa mwaka 1911 kwa lengo la kupigania haki na usawa wa wanawake duniani.
Alitolea mfano mafanikio ya Rais Samia kama uthibitisho kuwa mwanamke ana uwezo mkubwa wa kuongoza na kushinda changamoto mbalimbali za maisha, huku akimnukuu aliyekuwa Mke wa Rais wa zamani wa Marekani, Michelle Obama akisisitiza kuwa wanawake wanapaswa kuendelea kujiamini na kusonga mbele licha ya changamoto wanazokutana nazo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amepongezwa kwa juhudi zake za kuhamasisha wanawake kushiriki kikamilifu katika nyanja mbalimbali za maendeleo, hususan katika sekta za utalii na uhifadhi, hatua inayochangia kuongeza usawa wa kijinsia na kuwajengea wanawake ujasiri wa kushika nafasi za uongozi.
Pongezi hizo zimetolewa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Sekela Mwangota, ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini
Mwangota amesema uongozi wa Rais Samia umefungua fursa zaidi kwa wanawake kuamini uwezo wao, kujitokeza katika nafasi mbalimbali za uongozi na kushiriki kikamilifu katika maamuzi muhimu ya maendeleo ndani ya taasisi na jamii kwa ujumla.
Alitoa kauli hiyo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Machi 8, 2026 katika ukumbi wa Mafao House jijini Arusha, ambapo wanawake wa TANAPA waliungana kuadhimisha siku hiyo muhimu.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwangota alisema siku hiyo ni fursa ya kutambua mchango mkubwa wa wanawake katika maendeleo ya jamii,
Katika hafla hiyo iliyobeba ujumbe wa “Nguvu ya Mwanamke wa TANAPA, Fahari ya Uhifadhi na Utalii,” Mwangota alimkaribisha Mtaalamu wa Itifaki na Mwanadiplomasia Mwandamizi, Omary Kashera, kutoa mada kuhusu nafasi ya wanawake katika uongozi na maendeleo.
Kashera alisema kuwa Siku ya Wanawake Duniani ilianzishwa mwaka 1911 kwa lengo la kupigania haki na usawa wa wanawake duniani.
Alitolea mfano mafanikio ya Rais Samia kama uthibitisho kuwa mwanamke ana uwezo mkubwa wa kuongoza na kushinda changamoto mbalimbali za maisha, huku akimnukuu aliyekuwa Mke wa Rais wa zamani wa Marekani, Michelle Obama akisisitiza kuwa wanawake wanapaswa kuendelea kujiamini na kusonga mbele licha ya changamoto wanazokutana nazo.



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...