Timu ya Mchezo wa kuvuta kamba ya Wanaume na wanawake ya Wizara ya Maliasili na Utalii imeiburuza  bila huruma timu pinzani za Utamaduni na Mashtaka 2-0 katika michezo ya Mei Mosi iliyoanza kurindima Mkoani Njombe. 

Akizungumza baada ya michuano hiyo, Mwenyekiti wa Maliasili Sports Club Bw. Elia Mutalemwa amesema kuwa, siri ya ushindi huo ni maandalizi mazuri chini ya uangalizi wa viongozi wa Wizara. 

Kocha wa timu hiyo Bw. Gabriel Michael  amefafanua kuwa ushindi wa 2-0 wa timu ya Maliasili Wanawake  Kamba dhidi ya timu ya Utamaduni, ulikuwa mwepesi kwao kutokana na uwekezaji mkubwa  uliofanyika kwa wachezaji wake. 

Amewashukuru wakazi wa Njombe kwa kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao jambo lililo inua ari kubwa kwa wachezaji na kuipelekea pia timu ya Maliasili Wanaume kuiburaza bila huruma 2-0 timu ya Mashtaka na kuifanya iondoke uwanjani kwa majonzi makubwa. 

Naye Bi. Neema Mkinga mkazi wa Makambako amesema amevutiwa na Michezo hiyo hasa namna timu zilivyojipanga hususan timu za Maliasili na Utalii. 

Michuano hiyo ya kuelekea maadhimisho ya Sikuku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yameanza rasmi Mkoani Njombe huku kila timu ikijigamba kuibuka na ushindi thidi ya timu nyingine.





 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...