Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Ndg. Abdi Mahmoud Abdi, ameridhishwa na hatua ya ujenzi wa Hospitali ya Nungwi, Mkoa wa Kaskazini ‘A’, akisema mradi huo utasaidia kutatua changamoto mbalimbali za huduma za afya kwa wananchi wa jimbo hilo.

Ndg. Abdi amesema ujenzi wa hospitali hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, yenye lengo la kuboresha huduma za afya na kuzisogeza karibu zaidi na wananchi.

Aidha, amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na viongozi wao kuanzia ngazi ya jimbo hadi taifa, katika kuhakikisha huduma za kijamii, hususan afya, zinaendelea kuboreshwa na kusogezwa karibu na wananchi.

Kwa upande wake, mkandarasi wa mradi huo amesema ujenzi wa kituo hicho cha afya chenye ghorofa mbili umefikia asilimia 70 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba mwaka huu.






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...