2009
no image

HAVE A GREAT AND WONDERFUL 2010
Nimeona niwatakie HAPP NEW YEAR Watanzania wenzangu, pamoja na kufiwa na Mpendwa wetu Simba wa Vita sisi wengine tulio hai na tumshukuru Mungu. Mola aiweke peponi roho ya Mzee Rashidi Mfaume Kawawa - Amina.

Naomba nitume wimbo wa ABBA Group 'Happy New Year' kwa wadau wote wa Globu ya Jamii popote mlipo duniani
mdau wa Indiana USA
saria1974@gmail.com

Mkuu Mkoa wa Dar es salaam, William Lukuvi akimfariji mke wa Marehemu Rashidi Mfaume Kawawa, Asina Kawawa, wakati alipoitembelea familia ya marehemu nyumbani kwa marehemu Madale leo jioni
Katibu Mkuu wa CCM, Yusu Makamba (kushoto) akimlilia Mzee Rashid Kawawa wakati alipokwenda nyumbani kwa marehemu, Madale jijini Dar leo jioni.

katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba akimfariji Zainabu Kawawa mtoto wa Simba wa Vita marehemu, Rashidi kawawa, Madale leo jioni.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, William Lukuvi akimpa pole Mh. Vita Kawawa Mbunge wa Namtumbo, Songea) ambaye mtoto wa Marehemu Rashid Kawawa nyumbani kwa marehemu Madale, jijini Dar leo jioni.

RATIBA YA MAZISHI YA SIMBA WA VITA

Mazishi ya Simba wa Vita Mzee Rashid Mfaume Kawawa yanatarajiwa kufanyika siku ya jumamosi nyumbani kwa marehemu Madale jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa ratiba fupi iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa dar es salaam, Mh. William Lukuvi amesema jioni hii kuwa siku ya ijumaa mwili wa marehemu utapelekwa katika viwanja vya Karimjee kwa ajili ya wananchi kutoa heshima za mwisho.
Mh Lukuvi amewataka wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kuanzia majira ya saa saba mchana kumuaga Simba wa Vita.


Meneja Mafunzo wa Kampuni ya Swissport Tanzania Ltd, Nyasso Gama (kulia), akikata utepe kumkabidhi Ofisa Mfawidhi wa Makao ya Taifa ya Kurasini ya Kulelea Watoto Yatima, Margareth Mkandawile msaada wa mbuzi na vyakula mbalimbali vyenye thamani ya sh. 720,000 katika hafla iliyofanyika sambamba na kukabidhi Jengo lililojengwa kwa gharama ya sh. milioni 48 zilizochangwa na wafanyakazi wa Swissoprt. Hafla hiyo ilifanyika katika makao hayo, Dar
Watoto Yatima wanaolelewa katika Makao ya Taifa ya Kurasini, Dar es Salaam, wakiimba wimbo wa kuisifia Kampuni ya Swissport Tanzania Ltd, kwa kukabidhi jengo lililojengwa kwa gharama ya sh. milioni 48 zilizochangwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo. Hafla ya kukabidhi jengo hilo ilifanyika katika Makao hao jana.

Meneja Mafunzo wa Kampuni ya Swissport Tanzania Ltd, Nyasso Gama (kulia) akimkabidhi Ofisa Mfawidhi wa Makao ya Taifa ya Kurasini ya Kulelea Watoto Yatima, Margareth Mkandawile msaada wa vyakula mbalimbali
msaada wa vyakula kwa kituo hicho toka Swissport
Jengo lililojengwa kwa gharama ya sh. milioni 48 zilizochangwa na wafanyakazi wa Swissoprt, ambalo lina vyumba viwili vya madarasa, Ofisi ya waalimu na vyoo


Dear Michuzi,
Wishing you a Happy and Prosperous New Year 2010 and remembering those who could not make it thru.

Naomba wawekee wadau wa Globu ya Jamii hii picha ya Baraza la kwanza la Mawaziri wa Tanganyika mnamo mwaka 1961. Inaonyesha kabisa kwamba Mzee Kawawa ndiye aliyekuwa peke yake amebaki kati ya waasisi hao.

RIP Sima wa Vita Mzee Rashidi Mfaume Kawawa.
Sisi tulikupenda lakini Mola kakupenda zaid - Amin
Mdau SM
no image

KWA MUJIBU WA TAARIFA AMBAZO GLOBU YA JAMII IMEZIPATA NI KWAMBA SIMBA WA VITA HAYATI MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA ATAZIKWA SIKU YA JUMAMOSI HUKO NYUMBANI KWAKE MADALE WILAYA YA KINONDONI KWA HESHIMA ZOTE ZA KITAIFA.

VIONGOZI KADHAA WA NCHI ZA NJE WANATARAJIWA KUHUDHURIA MAZISHI YA SHUJAA HUYU AMBAYE ATAKUMBUKWA KWA UADILIFU WAKE NA KUJITOA MUHANGA KATIKA KUGOMBEA UHURU NA PIA UKOMBOZI WA BARA LA AFRIKA. HABARI ZAIDI ZITAKUJA KADRI ZITAVYOPATIKANA

The late Mzee Kalunga

We, the Kalunga’s family, wish to convey our sincere gratitude to all relatives, friends &neighbors for their moral, financial& material support during the time of bereavement.

Special thanks go to St .Peters Church Priests &choirs, Karoli Lwanga members, Tanganyika law society members, Hon. Judges and Advocates, Muhimbili, Khan& CCBRT Hospitals Staff.

Since it is not possible to thank each of everyone who assisted us during the difficult moment, Please accept this as the family’s sincere message of appreciation. Your memory will forever remain in our hearts. We thank God for the time we spent with you.

Dear Baba in God’s hands you rest,
in our hearts forever you will live and remain forever.
Rest in peace.
Coach Stewart Hall,
currently with Pune FC of India
A former national coach of Trinidad & Tobago and St. Vincent & The Grenades, Stewart Hall from England, is eyeing Marcio Maximo's Taifa Stars post.

Hall is the coach of coaches respected by Roy Keane, Gareth Southgate, Steve Staunton and Tony Adams. He is the man who trained millionaire professional, Fulham's Andrew Johnson and Craig Fagan of Hull City.

In 2007, Stewart was in Tanzania for coaching interview but lady luck was on Maximo. The Brazillian coach's contract with Taifa Stars expires in July 2010. Reports have it that he might leave in March next year.

Then he came back along with John Barnes, Warren Barton and Les Ferdinand for Tanzania's football development charity game.

Yesterday, he told BBC that he had just turned down an offer from one West African country for security reasons. Soon Stewart it is expected to be available to tell Tanzanians about his coaching package.
RAIS JAKAYA KIKWETE AKITANGAZA RASMI KIFO CHA SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA LEO IKULU JIJINI DAR
WANAHABARI WAKIMSIKILIZA AIS JAKAYA KIKWETE AKITANGAZA RASMI LEO KUHUSU KIFO CHA SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA MUDA MFUPI ULIOPITA IKULU, DAR. JK AMETANGAZA PIA SIKU SABA ZA MAOMBOLEZO KITAIFA AMBAPO BENDERA ZITAPEPEA NUSU MLINGOTI NCHI NZIMA. MAANDALIZI YA MAZIKO YANAENDELEA NA JK KAOMBA SUBIRA NA ITATANGAZWA WAKATI WOWOTE MAMBO YAKISHAKAMILIKA
RAIS JAKAYA KIKWETE AKIONGEA NA MWANASIASA MKONGWE MZEE KINGUNGE NGOMBARE MWIRU BAAD A YA KUTANGAZA RASMI KIFO CHA SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA LEO IKULU JIJINI DAR

KIPENZI CHETU SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA HATUNAYE TENA.
MZEE KAWAWA AMETUTOKA LEO ASUBUHI KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI ALIKOLAZWA TOKEA JANA BAADA YA KUPATA MATATIZO YA KIAFYA.
ALIZALIWA LIWALE MWAKA 1926 AMBAPO BAADA YA KUSHIKA NYADHIFA MBALI MBALI ALIKUWA WAZIRI MKUU KUANZIA JANUARI 22, 1962 HADI FEBRUARI 13, 1977 AKIFUATIWA NA HAYATI EDWARD MORINGE SOKOINE. BAADAYE ALIKUWA KATIBU MKUU WA CCM KABLA YA KUSTAAFU.
RAIS JAKAYA KIKWETE AKITETA NA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA KATIKA MOJAWAPO YA PICHA ZA MWISHO ZA KUTUMIMIKIA TAIFA ENZI ZA UHAI WAKE
MZEE KAWAWA AKIWA MMOJA WA WAKUU WALIOPIGANIA UHURU AKIWA KATIKA TAFRIJA YA KUSHEREHEKEA UHURU WA TANGANYIKA. YEYE NA MWALIMU WALIKUWA WATU WA KARIBU NA WALILITUMIKIA TAIFA KWA MOYO WOTE
MZEE KAWAWA AKIWA NA MKEWE BUNGENI DODOMA. PAMOJA NA UTU UZIMA DAIMA ALKIKUWA MSTARI WA MBELE KULITUMIKIA TAIFA
MZEE KAWAWA AKITUNUKIWA TUZO YA AMANI YA MARTIN LUTHER KING NA BALOZI WA MAREKANI NCHINI
MZEE KAWAWA ALIKUWA HAKOSEKANI KWENYE VIKAO MUHIMU VYA CCM
MZEE KAWAWA ALIKUWA RAFIKI WA KARIBU NA WANAHABARI. HAPA AKIWA NA CHARLES HILARY WA BBC WAKATI AKIWA JIJINI LONDON, UINGEREZA, KWA MATIBABU
MZEE KAWAWA ALIKUWA MPENZI MKUBWA WA MICHEZO. HAPA AKIWA REFA KATIKA MCHEZO WA WABUNGE NA MAWAZIRI ENZI HIZO
MZEE KAWAWA AKIWA NA TAIFA STARS
MZEE KAWAWA AKIWA MGENI RASMI KWENYE ONESHO LA MISS TANZANIA AMBAPO MSHINDI ALIIBUKA RICHA ADHIA ALIYE NYUMA YAKE
MZEE KAWAWA AKIWA NA MWALIMU NA RAIS WA ZANZIBAR ENZI HIZO MZEE ABOUD JUMBE. PEMBENI NI RAIS SAMORA MACHEL WA MSUMBUJI
AKIWA KAMA KIONGOZI WA VITENDO MZEE KAWAWA ALIKUWA MIONGONI MWA WATU WA KWANZA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA MUJIBU WA SHERIA MARA TU LILIPOANZA RASMI
MZEE KAWAWA AKIWA NA MWALIMU PAMOJA NA KIONGOZI WA DINI WA DHEHEBU LA ISMAILIA DUNIANI H.H. THE AGA KHAN


aina ya bango litalotumika katika kampeni ya TTB na TFF ya kuhamasisha umma kwenda kuishangilia Taifa Stars itapocheza na Ivory Coast January 4, 2010 katika uwanja wa taifa jijini Dar
Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya FIFA 2010 Mh. Dr. Shukuru Kawambwa akiongea leo na wanahabari ofisini kwake jijini Dar kuhusu maandalizi ya kamati hiyo na kampeni ya kuhamasisha nchi washiriki wa michuano ya Kombe la Dunia kupitia hapa nchini ama kuweka kambi kwa ajili ya maandalizi kuelekea nchini Afrika kusini katika michuano ya Kombe la Dunia inayotarajiwa kufanyika mwakani nchini humo. Wengine toka kulia ni Dan Mrutu Kutoka Baraza la Biashara na Frolence Turuka katibu mkuu wa wizara ya Sayansi Teknolojia na Elimu ya juu

Rais wa TFF akifafanua jambo wakati wa mkutano huo. Wengine ni Dk Shukuru Kawamba, Mh. Frolence Turuka na Bw. Dan Mrutu.

BILIONI SABA ZATENGWA KWA KAMPENI YA FIFA WORLD CUP 2010
Jumla ya shilingi Bilioni 7 zimetengwa kwa ajili ya kugharamia kampeni ya kuhamasisha nchi washiriki wa michuano ya Kombe la Dunia kupitia hapa nchini ama kuweka kambi kwa ajili ya maandalizi kuelekea nchini Afrika kusini katika michuano ya Kombe la Dunia inayotarajiwa kufanyika mwakani nchini humo.

Waziri wa Maendeleo ya Miundombinu, Dk Shukuru Kawamba, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya FIFA 2010, amesema leo pesa hiyo itatumika kwa matangazo katika vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na vya kimataifa, ulinzi na kuzigharamia timu na wageni.


Dk Kawambwa kasema televisheni za Supersport kutoka Afrika Kusini na SunVideo kutoka Brazil ziko tayari kufanya kazi ya kutangaza mambo mbalimbali yanayohusu Tanzania na maadalizi ya timu mbalimbali zitakazokuwa hapa nchini. Vyombo vingine ni BBC, Dautchwelle, Al jazeera VOA na vingine vingi.

Ameelezaa kuwa kampeni hiyo itaanza mapema wakati Timu ya Ivory Coast itapowasili nchini Januari 2 na kucheza na timu ya taifa Taifa Stars januari 4 na pia itacheza na timu ya Rwanda Januari 7 ambayo itawasili hapa nchini Januari 6 kwa ajili ya mchezo huo.

Rais wa Shirikisho la Mpira nchini Leodegar Chilla Tenga amesema tayari TFF wana mawasiliano na nchi nyingi zilizofanikiwa kuingia kwenye Fainali za Kombe la Dunia chini Afrika Kusini.

Tenga kazitaja nchi walizokwisha wasiliana nazo kuwa ni pamoja na Ujerumani, Italy, Denmark, New Zealand, Brazil, Australia, Korea Kaskazini,Japan, Argelia na Nigeria na nchi zingine ambazo bado mazungumzo yanaendelea.

Wakati huo huo Bodi ya Utalii (TTB) ikishirikiana na TFF wameanza kampeni ya kuhamasisha umma wa watanzania kwenda kuiunga mkono na kuishangilia Taifa Stars wakati wa mechi yake na Ivory Coast katika mchezo wa kirafiki Januari 4 kwenye uwanja wa Taifa.

Katika kampeni hii kutakuwa na mabango makubwa na madogo ya matangazo, vipeperushi, matangazo ya redio, magazeti na televisheni pamoja na vijarida ili kuhamasisha mashabiki kwenda kushangilia timu yao.

JK na mkewe Mama Salma Kikwete wakimjulia hali Mzee Rashid Mfaume Kawawa aliyelazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili leo jioni. Kulia ni profesa Victor Mwafongo. Mzee Kawawa alipelekwa hapo Muhimbili baada ya kujisikia vibaya na kupelekwa hapo kwa kuangaliwa. Vipimo vinaendelea kujua anasumbuliwa na nini na hali yake ni stable.
Picha na Freddy Maro wa Ikulu.



A woman suffering from skin disorder due to sking lightening creams

THE zeal to look beautiful and a colonial mentality that white skin is superior is fast driving Tanzanian women into their graves as they risk their lives by using skin lightening creams that in the end turn lethal.

The problem is not only confined to Tanzania as selling of whitening creams is a lucrative business in Africa worth millions of US dollars a year. In some countries that allow the use of these lethal substances, shelves in pharmacies are stacked high with lotions, creams and soaps all promising to make women whiter and supposedly more beautiful.

But, in countries like Tanzania, where the use and importation of skin lightening creams is banned, the business is thriving as these dangerous creams are smuggled into the country while dealers on the other hand are discrete.

Read the rest of this mkorogo story:
no image
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), leo ilimfikisha katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Mkuu wa idara ya Ulinzi katika Shule za St.Marys, kwa tuhuma za kudai rushwa ya Ngono.

Mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo Omari Kingwele, Mwanasheria kutoka katika Taasisi hiyo Sophia Gura, alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Eustace Mrefu mkazi wa jiji la Dar es salaam.

Akimsomea shitaka linalomkabili katika kesi hiyo, Gura alidai mahakamani hapo kuwa Mrefu alitenda kosa hilo Aprili 28, 2008 kwenye nyumba ya kulala wageni ya Chem Chem iliyoko maeneo ya Tabata Dar es salaam, ambapo anadaiwa kudai rushwa hiyo kwa Celina Peter.

Mshtakiwa huyo anadaiwa kudai rushwa hiyo kwa msichana huyo, kwa kumhadaa kuwa angemtafutia kazi katika shule hizo au katika ofisi zingine, kwani msichana huyo alimuomba amsaidie kwa hilo.

Hata hivyo mshitakiwa huyo alikana kuhusika na tuhuma hizo, ambapo alirudishwa rumande baada ya kukosa wadhamini wawili waliotakiwa kumdamini kwa kusahini hati ya dhamana yenye thamani ya Shilingi laki 5 kila mmoja.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi Januri 14 mwaka huu, itakapofika mahakamani hapo kwaajili ya kutajwa.
MAKAZI YA GAVANA WA BENKI KUU

TAARIFA KUHUSU UJENZI WA MAKAZI YA VIONGOZI WAKUU WA BENKI KUU YA TANZANIA

GAVANA WA Benki Kuu na manaibu wake kwa mujibu wa mikataba ya kazi zao, wanastahili kupewa nyumba ya kuishi kila mmoja. Hapo awali Gavana alikuwa anaishi Barabara ya Mahando kiwanja namba 387Masaki na Naibu Gavana Barabara ya Msese kiwanja Namba 43.

Awali Benki Kuu ilikuwa na viongozi wakuu wawili, Gavana na Naibu wake mmoja. Baada ya mabadiliko ya Sheria ya mwaka 2006, Benki Kuu ina viongozi wakuu wanne; Gavana na Manaibu wake watatu. Kila mmoja wao, kwa mikataba iliyowekwa anastahili kupata nyumba ya kuishi.

Mwaka 2006, kabla ya uteuzi wa viongozi wa sasa wa juu, Benki Kuu ilifanya uamuzi wa kujenga nyumba mbili zaidi kwa makazi ya viongozi walioongezeka. Iliamuliwa nyumba hizi zijengwe kiwanja namba 57 Barabara ya Mtwara Crescent na kiwanja namba 12 Barabara ya Tumbawe maeneo ya Oysterbay.Viwanja vyote viwili vilikuwa ni mali ya Benki Kuu vilivyokuwa na magofu yaliyopigwa marufuku kuishi wanadamu (condemned).

Timu ya wataalamu waelekezi ikiongozwa na M/S SKY Architects Consultants iliajiriwa kutengeneza michoro na ramani za nyumba hizo. Michoro miwili ilichaguliwa, moja kwa kila nyumba ili wataalamu hao watengeneze ramani kamili ya ujenzi. Nyumba zote mbili zilipangwa ziwe za ghorofa moja, vyumba vitano vya kulala, wenyeji na wageni, sebule ya wageni, sebule ya familia, mahali pa kulia na vyoo na mabafu yanayoendana na idadi ya vyumba. Majengo ya nje ni pamoja na nyumba ya kuishi watumishi, gereji ya magari, bwawa dogo la kuogelea, ukuta na vyombo vya usalama na kibanda cha walinzi.

Huduma zilizogharimiwa katika ujenzi wa nyumba hizi ni pamoja na mashine ya umeme (generator), mashine ya kupoza hewa na matenki ya kuhifadhi maji. Wakati huohuo, shughuli zingine zilizofanyika ilikuwa ni kutengeneza mahali pa kuegesha magari pamoja na bustani.

Wataalamu hawa baada ya uchoraji huu walifanya tathmini ya vifaa vinavyohitajika na maelekezo kwa wazabuni ili itumike kualika zabuni. Taratibu zote za manunuzi zilifuata sheria ya manunuzi katika kuwaalika wazabuni na kuteua wakandarasi. Kila nyumba ilikuwa ni mradi unaojitegemea na kila moja ilifanyiwa zabuni peke yake.

Izingatiwe kuwa ujenzi wa nyumba hizi ulipangwa na kuamuliwa kabla ya uteuzi wa Profesa Benno Ndulu kujiunga na Benki Kuu Septemba 2007.

Tangazo la kuwaalika wazabuni kwenye kiwanja namba 12 Barabara ya Tumbawe lilichaapishwa katika gazeti la Daily News la Februari 26,2008.Wakandarasi wote wa daraja la pili au la juu zaidi walialikwa kuwasilisha zabuni na walitakiwa kulipa ada ya shilingi 50,000. Wakandarasi 12 walituma maombi na kuchukua hati za zabuni.Lakini kati ya hao 10, waliwasilisha maombi yao kabla ya kufikia tamati ya kupokelewa maombi hayo Machi 25,2008.

Zabuni hizi zilifunguliwa na Bodi ya Zabuni ya Benki Kuu na kufanyiwa tathimini ikishirikisha mtaalamu mwelekezi wa mradi huo na Idara ya Miliki ya Benki Kuu. Mapendekezo kutoka kwa wakandarasi yalikuwa na viwango vya gharama kuanzia Shilingi 1,399,184,549.00 hadi shilingi 1,847,763,537.00 kwa kiwango cha juu. Baada ya tathmini ya zabuni hizo na kufanya masahihisho ya tarakimu zilizowasilishwa, mzabuni aliyeshinda kwa kuwa na gharama ya chini kuliko wote alikuwa ni M/S Eletrics International Co. Limited. Gharama yake baada ya masahihisho ilikuwa ni Shilingi 1,274,295,025.26.

Taarifa ya tathimini hiyo ilipitia tena kwenye Bodi ya Wazabuni na ndipo ilipofikia uamuzi wa kumteua M/S Eletrics International Co. Limited kwa bei ambayo haitabadilika (fixed price) ya Shilingi 1,274,295,025.26 ya kukamilisha ujenzi huu katika wiki 32.Mkataba wa ujenzi na mkandarasi huyo ulitiwa sahihi Juni 03,2008 na kazi ya ujenzi ikaanza mara moja. Mkandarasi huyu aliteuliwa na Bodi Zabuni (DSM) ya Benki Kuu ikaridhia kuwa M/S Remco (International) Limited ishughulikie maswala aya vipoza hewa; M/s Ginde EAP Services Ltd ishughulikie maswala ya maji safi, mabomba na maji taka na M/s Pomy Engineering Co.Ltd ishughulikie maswala ya umeme. Makampuni yote hayo yamesajiliwa Tanzania.

Wazabuni wa nyumba Namba 57 Mtwara Crescent nao pia walialikwa kwa mfumo huohuo wa ushindani wakianza na wakandarasi watano (5) ambao waliwasilisha maombi yao na kuishia na uteuzi wa M/s Holtan Builders Ltd ambayo gharama yake ya Shilingi 1,272,348,512.00 (fixed price) ilikuwa ni ya chini kuwashinda wengine na makubaliano ya kukamilisha ujenzi katika muda wa wiki 24. Mkandarasi huyo alitumia kampuni zifuatazo kwa shughuli zingine: M/s Jandu Construction & Plumbers Ltd kwa shughuli za mabomba, maji safi, na maji taka, M/s Barkley Electrical Contractors Ltd kwa maswala ya umeme na M/s Remco (International) Ltd kwa shughuli za vipoza hewa. Mkandarasi ndiye mlipaji wa gharama za shughuli hizi zote zinalipiwa kutokana na gharama ileile iliyokubalika kwa mkandarasi mkuu.

Watendaji wote wa miradi hii wanaonyeshwa kwenye mabango ambayo bado yapo kwenye viwanja hivyo. Uteuzi wa Gavana Ndulu, Manaibu Gavana, Dkt. Enos Bukuku na Bw.Lila Mkila ulifanyika wakati mipango ya awali ya kujenga nyumba hizi

ilikuwa imeshaanza. Benki Kuu ilikodisha nyumba mbili, mojakiwanja namba 480 Barabara ya Bray, Masaki na nyingine kiwanja namba 591,Msasani Peninsular kwa matumizi ya viongozi hao wawili ambao walikuwa bado wanaishi kwenye nyumba zao mbali na ofisi.

Kati ya Oktoba 2007 aliporipoti kazini kama Naibu Gavana hadi Aprili 2008, Profesa Ndulu aliishi kwenye nyumba yake iliyoko Mbezi Beach, na Naibu Gavana Mkila naye pia aliishi nyumbani kwake kabla ya kuhamia kwenye nyumba hizi zilizokodishwa.

Benki Kuu iliamua kumhamisha Naibu Gavana Juma Reli kwenda Barabara ya Mahando Masaki ili kuruhusu matengenezo ya nyumba aliyokuwa anaishi Kinondoni Barabara ya Msese. Naibu Gavana Dkt.Bukuku anaishi kwenye nyumba yake na Benki Kuu inatoa posho ya nyumba kulingana na mkataba.

Nyumba hizo mbili zilizojengwa chini ya miradi iliyotajwa, sasa hivi zimekamilika.Gavana wa Benki Kuu, Profesa Ndulu alihamia nyumba namba 12 Barabara ya Tumbawe Desemba 17,2009 na Naibu Gavana Mkila alihamia nyumba namba 57 Mtwara Crescent Desemba 4,2009

Kama ilivyo kiutaratibu, ukaguzi wa mahesabu yanayohusu miradi hiyo utafanyika kisheria. Kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya mwaka 2006, Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) ndiye mkaguzi wa mahesabu ya Benki Kuu; ambaye ameanza kufanya kazi hii tangu mwaka 2007. Yeye ameiteua kampuni ya Ernst & Young kama wakaguzi wa kumsaidia kutekeleza jukumu hili.

IMETOLEWA NA IDARA YA UHUSIANO NA UMMA NA ITIFAKI
BENKI KUU YA TANZANIA
SEPTEMBA 30, 2009
BOT GOVERNOR'S OFFICIAL RESIDENCE

CONSTRUCTION OF THE BANK OF TANZANIA EXECUTIVE RESIDENCES

Bank of Tanzania Executive officers are entitled to official residence provided by the Bank. Initially the Bank used to have only two executive officers, the Governor and one Deputy Governor. The Governor was living at BOT house No. 387 Mahando Street and Deputy Governor at BOT house No. 43 Msese Road. As a result of the changes made in section 8 of the Bank of Tanzania Act, 2006, the Bank has now four Executives, the Governor and three Deputy Governors, for whom it is obliged to provide official accommodation.

In 2006, in advance of the presidential appointment of the current office bearers, the Bank decided to construct two additional executive accommodations, one on plot No. 12 Tumbawe Road and another on plot No. 57 Mtwara Crescent at Oysterbay, Dar es Salaam. A team of consultants led by M/S SKY Architects Consultants was engaged to provide schematic drawings that were reviewed by the Bank and two of these, one for each plot, were selected for detailed design stage.


Each residence was designed to be a one storey building with five bedrooms, visitors lounge, family lounge, dining area and associated service rooms. The outbuildings include servant’s quarter, car ports, swimming pool, boundary wall, security systems and guard house. Services include power generator, central cooling system and water storage facilities while external works include landscaping and paved car park.

The consultants then prepared bills of quantities and technical specification that were compiled to form tender documents ready for tender process. All procedures in line with procurement laws and regulation were adhered to, when determining the cost of each of the residences as well as in selecting contractors and sub contractors. Each residence was considered as an independent project and a separate tender process was carried out for each one.

It is important for the public to know that, the planning and decision to have these houses constructed was done before Prof Benno Ndulu was appointed at the Bank of Tanzania.

Tenderers for works at plot No. 12 Tumbawe Street were invited using competitive open tender advertised on the Daily News of 26th February 2008. Interested contractors of class II and above were invited to apply for tender document and were instructed to pay non-refundable tender fee of Tshs 50,000/=.

A total of 12 contractors applied and collected the tender documents, but only 10 submitted their bids before deadline, 25th March 2008. The received tenders were opened by BOT Tender Board and forwarded to Project Consultant via the Bank of Tanzania Estate Management Department for evaluation. Tender results read during tender opening ranged from the lowest tender price of Tshs 1,399,184,549.00 to the highest price of Tshs 1,847,763,537.00.

After tender evaluation, which involved preliminary examination of tender, arithmetic correction and detailed analysis, the lowest evaluated bidder was determined to be M/s Electrics International Co. Limited at a corrected tender price of Tshs 1,274,295,025.26. Evaluation report was deliberated by BOT Tender Board and it was approved to award construction works to M/s Electrics International Co. Limited at a fixed contract price of Tshs 1,274,295,025.26 and 32 weeks completion period.

Contract agreement between the Bank and the contractor was signed on 3rd June 2008 and construction works started immediately thereafter. Subcontractors for specialized works were nominated and approved by the BOT Tender Board. These included M/s Remco (International) Ltd for Air Conditioning installation, M/s Ginde EAP Services Ltd for plumbing and drainage systems and M/s Pomy Engineering Co. Ltd for Electrical installations. All these companies are registered in Tanzania.

Tenderers for house no. 57 Mtwara Crescent were invited through a competitive tender method where 5 short-listed contractors were invited to collect tender documents and bid for work. Submitted tenders went through the same tender process detailed above that resulted into M/s Holtan Builders Ltd being determined the lowest evaluated bidder at Tshs 1,272,348,512.00 and 24 weeks completion period.

Subcontractor nominated and approved in this case were M/s Jandu Construction & Plumbers Ltd for plumbing and drainage systems, M/s Barkley Electrical Contractors Ltd for electrical installation and M/s Remco (International) Ltd for Air Conditioning installation. The cost for specialized works undertaken by subcontractors for each site is included on the fixed contract prices for respective main contractor. Likewise, lists of project parties for both works are displayed on the sign boards that are still erected at the front side of respective plots.

While the two projects were still on preliminarily stages, appointment of the three new executive officers to Bank of Tanzania was completed. The Bank was thus compelled to rent two residential houses one on plot No. 480 Bray Road Masaki and another on plot No. 591 at Msasani Peninsular.

One house was allocated to Professor Benno Ndulu, by then the first Deputy Governor, and another to Deputy Governor Lila Mkila. Prior to moving to this rented house; between October 2007 and April 2008, Prof Ndulu lived in his own house in Mbezi Beach. Likewise Deputy Governor Mkila stayed in his own house before moving to the rented premise.

These movements were to facilitate easy access to the office in light of traffic congestion in the city. It was decided to relocate Deputy Governor Juma Reli to house No. 387 Mahando Street to give way for planned refurbishment required at house No. 43 Msese road. Deputy Governor Enos Bukuku is residing in his own private house, and is paid housing allowance in lieu of occupying official residence as entitled – pending the planned refurbishment of Plot No. 43 Msese road residence.

The construction of the two executive residences has now been completed. Both Governor Ndulu and Deputy Governor Mkila, who were residing in rented houses have relocated to the new Bank of Tanzania official residences. The Governor has relocated to house No. 12 Tumbawe Road since 17th December 2009 and Deputy Governor Mkila to house No. 57 Mtwara Crescent since 4th December 2009.

As it is with all other Bank of Tanzania projects, these too will be subject to the usual audit process. It might be important for the public to know that, as stipulated in the Bank of Tanzania Act 2006 the Controller and Auditor General (CAG) is the external auditor for the Bank. The CAG has retained the services of the Ernst and Young, an international audit firm to support the external audit work of the Bank.

Issued by Public Relations & Protocol Department
BANK OF TANZANIA
30TH DECEMBER 2009

no image
Bro NAKUPONGEZA SANA KWA KAZI YAKO YA KUTUJUZA YALIYOJIRI.

NAOMBA UNISAIDIE KWA KURUSHA HII KWENYE BLOG YAKO, NAMTAFUTA KAKA YANGU AITWAYE RAYMOND FRED MTOI TULIACHANA NAYE MWAKA 2000 ALIPOONDOKA KWENDA UK KWA MASOMO.
TULIWASILIANA KWA KIPINDI KIFUPI TU MARA BAADA YA KUFIKA HUKO UK THEN MAWASILIANO YAKAKATIKA MPAKA SASA SINA MAWASILIANO NAY. TAFADHALI KAMA KUNA MTU ANAYEMFAHAMU NA ANA CONTACT ZAKE AU KAMA MWENYEWE ATABAHATIKA KUSOMA BLOG HII NAOMBA AWASILIANE NAMI KWA e-mail hii nelangwa@yahoo.com

NI MIMI NAPENDAEL E.J.
MDAU EA DAR
Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa wa UVCCM, Gabriel Amos Makalla ( wapili kutoka kulia ) akisikiliza kwa makini hotuba ya mgeni rasmi ( hayupo pichani ) wakati wa kufungua mkutano mkuu wa Chipukizi ulioambanata na uchaguzi mkuu jana mjini Morogoro. Gabriel katika uchaguzi huo alichangukiwa kwa kishindo na wajumbe wa mkutano huo. Alipata zaidi ya asilimia 85 kwa kura 310 wakati wa pili alipata kura 19.
Baadhi ya wajumbe wa Chipukuzi Taifa katika mkutano mkuu kutoka Mkoa wa Ruvuma , Kagera na Mtwara wakiwa na wenzao wa Mikoa mingine ya Tanzania Bara na Visiwani wakisililiza hotuba ya mgeni rasmi wa Mkutano huo

Baadhi ya wapenzi na wakereketwa wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) na Umoja wa Vijana ( UVCCM) wakijipumzisha nje ya ukumbi wa Chuo Cha Ualimu Morogoro wakisubiri matokeo ya uchaguzi mkuu wa taifa wa Chipukizi ulifanyika mjini humo.



Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Mkoa wa Morogoro, Ahamed Msangi ( kushoto) akiwaongoza baadhi ya askari na wananchi katika ujenzi wa mahema kwa ajili ya kuishi watu waliokubwa na mafuriko na nyumba zao kibomolewa na mafuriko hayo , kwenye shule ya Msingi Mazinyungu ya Mjini Kilosa. Picha zote na mdau John Nditi
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Magomeni , Mjini Kilosa wakipita kwenye barabara iliyojaa maji ya mafuriko ya mvua pamoja na mizingo mikononi na vichwani kwenda kwenye makambi yaliyotengwa mjini humo
Vijana wa mjini Kilosa akitumia fursa ya mafuriko yaliyowaathiri wakazi wa Kata mbalimbali za mjini humo kuwasafirishia mizingo yao kwa kutumia usafiri wa mkokoteni na kutoza gharama ya sh: 1,000 hadi 2,000 kutokana na umbali. Mama akimwesha uji mwanae mchanga baada ya kufikishwa eneo la kambi iliyotengwa kwa ajili ya walioathiriwa na mafuriko ya maji katika mji wa Kilosa kwenye Shule ya Msingi ya Kilosa Town. Mafuriko hayo yaliaza tangu Desemba 26, mwaka huu.
Baadhi ya wananchi waliokubwa na mafuriko ya mvua kutoka Kata ya Mbumi, wakitelemsha vifaa vyaao kutoka katika gari la Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa mara baada ya kuwafikisha kambi ya Kilosa Klabu.
Kijana akikatisha katika barabara iliyojaa maji na baiskeli yake mgongoni
kambi ya dharura ya walioathirika na mafuriko kilosa
Mkazi wa Kilosa akielekea kwenye kambi ya dharura








Juu na chini ni gari aina ya fuso iliyokua inatokea Arusha kuelekea moshi ikiwa imeangushwa na mafuriko yaliyokuwa yamekatiza barabarani kutokana na mvua kubwa zilizokuwa zinanyesha mkoani Kilimanjaro fuso hiyo ilianguka katika mbele kidogo ya kijiji cha kwa Sadala wilayani Hai mkoani kilimanjaro. Mafuriko hayo yalizuia magari kupita kwa muda wa lisaa na nusu.(picha na Woinde Shizza)
Fuso likiwa limelala ubavu
maji yaendayo kasi yakikatisha barabara