HAVE A GREAT AND WONDERFUL 2010
Nimeona niwatakie HAPP NEW YEAR Watanzania wenzangu, pamoja na kufiwa na Mpendwa wetu Simba wa Vita sisi wengine tulio hai na tumshukuru Mungu. Mola aiweke peponi roho ya Mzee Rashidi Mfaume Kawawa - Amina.
Naomba nitume wimbo wa ABBA Group 'Happy New Year' kwa wadau wote wa Globu ya Jamii popote mlipo duniani
mdau wa Indiana USA
saria1974@gmail.com
RATIBA YA MAZISHI YA SIMBA WA VITA
Mazishi ya Simba wa Vita Mzee Rashid Mfaume Kawawa yanatarajiwa kufanyika siku ya jumamosi nyumbani kwa marehemu Madale jijini Dar es Salaam.

Wishing you a Happy and Prosperous New Year 2010 and remembering those who could not make it thru.
Naomba wawekee wadau wa Globu ya Jamii hii picha ya Baraza la kwanza la Mawaziri wa Tanganyika mnamo mwaka 1961. Inaonyesha kabisa kwamba Mzee Kawawa ndiye aliyekuwa peke yake amebaki kati ya waasisi hao.
RIP Sima wa Vita Mzee Rashidi Mfaume Kawawa.
KWA MUJIBU WA TAARIFA AMBAZO GLOBU YA JAMII IMEZIPATA NI KWAMBA SIMBA WA VITA HAYATI MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA ATAZIKWA SIKU YA JUMAMOSI HUKO NYUMBANI KWAKE MADALE WILAYA YA KINONDONI KWA HESHIMA ZOTE ZA KITAIFA.
VIONGOZI KADHAA WA NCHI ZA NJE WANATARAJIWA KUHUDHURIA MAZISHI YA SHUJAA HUYU AMBAYE ATAKUMBUKWA KWA UADILIFU WAKE NA KUJITOA MUHANGA KATIKA KUGOMBEA UHURU NA PIA UKOMBOZI WA BARA LA AFRIKA. HABARI ZAIDI ZITAKUJA KADRI ZITAVYOPATIKANA
in our hearts forever you will live and remain forever.
Rest in peace.
Hall is the coach of coaches respected by Roy Keane, Gareth Southgate, Steve Staunton and Tony Adams. He is the man who trained millionaire professional, Fulham's Andrew Johnson and Craig Fagan of Hull City.
In 2007, Stewart was in Tanzania for coaching interview but lady luck was on Maximo. The Brazillian coach's contract with Taifa Stars expires in July 2010. Reports have it that he might leave in March next year.
Then he came back along with John Barnes, Warren Barton and Les Ferdinand for Tanzania's football development charity game.
Yesterday, he told BBC that he had just turned down an offer from one West African country for security reasons. Soon Stewart it is expected to be available to tell Tanzanians about his coaching package.






Kolumba Mwingira is one of the members from the original Mawingu, which was responsible for starting swahili rap in the African continent.This is his new single (Usiondoke). Album is coming out soon

BILIONI SABA ZATENGWA KWA KAMPENI YA FIFA WORLD CUP 2010
Jumla ya shilingi Bilioni 7 zimetengwa kwa ajili ya kugharamia kampeni ya kuhamasisha nchi washiriki wa michuano ya Kombe la Dunia kupitia hapa nchini ama kuweka kambi kwa ajili ya maandalizi kuelekea nchini Afrika kusini katika michuano ya Kombe la Dunia inayotarajiwa kufanyika mwakani nchini humo.
Waziri wa Maendeleo ya Miundombinu, Dk Shukuru Kawamba, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya FIFA 2010, amesema leo pesa hiyo itatumika kwa matangazo katika vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na vya kimataifa, ulinzi na kuzigharamia timu na wageni.
Dk Kawambwa kasema televisheni za Supersport kutoka Afrika Kusini na SunVideo kutoka Brazil ziko tayari kufanya kazi ya kutangaza mambo mbalimbali yanayohusu Tanzania na maadalizi ya timu mbalimbali zitakazokuwa hapa nchini. Vyombo vingine ni BBC, Dautchwelle, Al jazeera VOA na vingine vingi.
Ameelezaa kuwa kampeni hiyo itaanza mapema wakati Timu ya Ivory Coast itapowasili nchini Januari 2 na kucheza na timu ya taifa Taifa Stars januari 4 na pia itacheza na timu ya Rwanda Januari 7 ambayo itawasili hapa nchini Januari 6 kwa ajili ya mchezo huo.
Rais wa Shirikisho la Mpira nchini Leodegar Chilla Tenga amesema tayari TFF wana mawasiliano na nchi nyingi zilizofanikiwa kuingia kwenye Fainali za Kombe la Dunia chini Afrika Kusini.
Tenga kazitaja nchi walizokwisha wasiliana nazo kuwa ni pamoja na Ujerumani, Italy, Denmark, New Zealand, Brazil, Australia, Korea Kaskazini,Japan, Argelia na Nigeria na nchi zingine ambazo bado mazungumzo yanaendelea.
Wakati huo huo Bodi ya Utalii (TTB) ikishirikiana na TFF wameanza kampeni ya kuhamasisha umma wa watanzania kwenda kuiunga mkono na kuishangilia Taifa Stars wakati wa mechi yake na Ivory Coast katika mchezo wa kirafiki Januari 4 kwenye uwanja wa Taifa.
Katika kampeni hii kutakuwa na mabango makubwa na madogo ya matangazo, vipeperushi, matangazo ya redio, magazeti na televisheni pamoja na vijarida ili kuhamasisha mashabiki kwenda kushangilia timu yao.
The problem is not only confined to Tanzania as selling of whitening creams is a lucrative business in Africa worth millions of US dollars a year. In some countries that allow the use of these lethal substances, shelves in pharmacies are stacked high with lotions, creams and soaps all promising to make women whiter and supposedly more beautiful.
Mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo Omari Kingwele, Mwanasheria kutoka katika Taasisi hiyo Sophia Gura, alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Eustace Mrefu mkazi wa jiji la Dar es salaam.
Akimsomea shitaka linalomkabili katika kesi hiyo, Gura alidai mahakamani hapo kuwa Mrefu alitenda kosa hilo Aprili 28, 2008 kwenye nyumba ya kulala wageni ya Chem Chem iliyoko maeneo ya Tabata Dar es salaam, ambapo anadaiwa kudai rushwa hiyo kwa Celina Peter.
Mshtakiwa huyo anadaiwa kudai rushwa hiyo kwa msichana huyo, kwa kumhadaa kuwa angemtafutia kazi katika shule hizo au katika ofisi zingine, kwani msichana huyo alimuomba amsaidie kwa hilo.
Hata hivyo mshitakiwa huyo alikana kuhusika na tuhuma hizo, ambapo alirudishwa rumande baada ya kukosa wadhamini wawili waliotakiwa kumdamini kwa kusahini hati ya dhamana yenye thamani ya Shilingi laki 5 kila mmoja.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Januri 14 mwaka huu, itakapofika mahakamani hapo kwaajili ya kutajwa.
TAARIFA KUHUSU UJENZI WA MAKAZI YA VIONGOZI WAKUU WA BENKI KUU YA TANZANIA
GAVANA WA Benki Kuu na manaibu wake kwa mujibu wa mikataba ya kazi zao, wanastahili kupewa nyumba ya kuishi kila mmoja. Hapo awali Gavana alikuwa anaishi Barabara ya Mahando kiwanja namba 387Masaki na Naibu Gavana Barabara ya Msese kiwanja Namba 43.
Awali Benki Kuu ilikuwa na viongozi wakuu wawili, Gavana na Naibu wake mmoja. Baada ya mabadiliko ya Sheria ya mwaka 2006, Benki Kuu ina viongozi wakuu wanne; Gavana na Manaibu wake watatu. Kila mmoja wao, kwa mikataba iliyowekwa anastahili kupata nyumba ya kuishi.
Mwaka 2006, kabla ya uteuzi wa viongozi wa sasa wa juu, Benki Kuu ilifanya uamuzi wa kujenga nyumba mbili zaidi kwa makazi ya viongozi walioongezeka. Iliamuliwa nyumba hizi zijengwe kiwanja namba 57 Barabara ya Mtwara Crescent na kiwanja namba 12 Barabara ya Tumbawe maeneo ya Oysterbay.Viwanja vyote viwili vilikuwa ni mali ya Benki Kuu vilivyokuwa na magofu yaliyopigwa marufuku kuishi wanadamu (condemned).
Timu ya wataalamu waelekezi ikiongozwa na M/S SKY Architects Consultants iliajiriwa kutengeneza michoro na ramani za nyumba hizo. Michoro miwili ilichaguliwa, moja kwa kila nyumba ili wataalamu hao watengeneze ramani kamili ya ujenzi. Nyumba zote mbili zilipangwa ziwe za ghorofa moja, vyumba vitano vya kulala, wenyeji na wageni, sebule ya wageni, sebule ya familia, mahali pa kulia na vyoo na mabafu yanayoendana na idadi ya vyumba. Majengo ya nje ni pamoja na nyumba ya kuishi watumishi, gereji ya magari, bwawa dogo la kuogelea, ukuta na vyombo vya usalama na kibanda cha walinzi.
Huduma zilizogharimiwa katika ujenzi wa nyumba hizi ni pamoja na mashine ya umeme (generator), mashine ya kupoza hewa na matenki ya kuhifadhi maji. Wakati huohuo, shughuli zingine zilizofanyika ilikuwa ni kutengeneza mahali pa kuegesha magari pamoja na bustani.
Wataalamu hawa baada ya uchoraji huu walifanya tathmini ya vifaa vinavyohitajika na maelekezo kwa wazabuni ili itumike kualika zabuni. Taratibu zote za manunuzi zilifuata sheria ya manunuzi katika kuwaalika wazabuni na kuteua wakandarasi. Kila nyumba ilikuwa ni mradi unaojitegemea na kila moja ilifanyiwa zabuni peke yake.
Izingatiwe kuwa ujenzi wa nyumba hizi ulipangwa na kuamuliwa kabla ya uteuzi wa Profesa Benno Ndulu kujiunga na Benki Kuu Septemba 2007.
Tangazo la kuwaalika wazabuni kwenye kiwanja namba 12 Barabara ya Tumbawe lilichaapishwa katika gazeti la Daily News la Februari 26,2008.Wakandarasi wote wa daraja la pili au la juu zaidi walialikwa kuwasilisha zabuni na walitakiwa kulipa ada ya shilingi 50,000. Wakandarasi 12 walituma maombi na kuchukua hati za zabuni.Lakini kati ya hao 10, waliwasilisha maombi yao kabla ya kufikia tamati ya kupokelewa maombi hayo Machi 25,2008.
Zabuni hizi zilifunguliwa na Bodi ya Zabuni ya Benki Kuu na kufanyiwa tathimini ikishirikisha mtaalamu mwelekezi wa mradi huo na Idara ya Miliki ya Benki Kuu. Mapendekezo kutoka kwa wakandarasi yalikuwa na viwango vya gharama kuanzia Shilingi 1,399,184,549.00 hadi shilingi 1,847,763,537.00 kwa kiwango cha juu. Baada ya tathmini ya zabuni hizo na kufanya masahihisho ya tarakimu zilizowasilishwa, mzabuni aliyeshinda kwa kuwa na gharama ya chini kuliko wote alikuwa ni M/S Eletrics International Co. Limited. Gharama yake baada ya masahihisho ilikuwa ni Shilingi 1,274,295,025.26.
Taarifa ya tathimini hiyo ilipitia tena kwenye Bodi ya Wazabuni na ndipo ilipofikia uamuzi wa kumteua M/S Eletrics International Co. Limited kwa bei ambayo haitabadilika (fixed price) ya Shilingi 1,274,295,025.26 ya kukamilisha ujenzi huu katika wiki 32.Mkataba wa ujenzi na mkandarasi huyo ulitiwa sahihi Juni 03,2008 na kazi ya ujenzi ikaanza mara moja. Mkandarasi huyu aliteuliwa na Bodi Zabuni (DSM) ya Benki Kuu ikaridhia kuwa M/S Remco (International) Limited ishughulikie maswala aya vipoza hewa; M/s Ginde EAP Services Ltd ishughulikie maswala ya maji safi, mabomba na maji taka na M/s Pomy Engineering Co.Ltd ishughulikie maswala ya umeme. Makampuni yote hayo yamesajiliwa Tanzania.
Wazabuni wa nyumba Namba 57 Mtwara Crescent nao pia walialikwa kwa mfumo huohuo wa ushindani wakianza na wakandarasi watano (5) ambao waliwasilisha maombi yao na kuishia na uteuzi wa M/s Holtan Builders Ltd ambayo gharama yake ya Shilingi 1,272,348,512.00 (fixed price) ilikuwa ni ya chini kuwashinda wengine na makubaliano ya kukamilisha ujenzi katika muda wa wiki 24. Mkandarasi huyo alitumia kampuni zifuatazo kwa shughuli zingine: M/s Jandu Construction & Plumbers Ltd kwa shughuli za mabomba, maji safi, na maji taka, M/s Barkley Electrical Contractors Ltd kwa maswala ya umeme na M/s Remco (International) Ltd kwa shughuli za vipoza hewa. Mkandarasi ndiye mlipaji wa gharama za shughuli hizi zote zinalipiwa kutokana na gharama ileile iliyokubalika kwa mkandarasi mkuu.
Watendaji wote wa miradi hii wanaonyeshwa kwenye mabango ambayo bado yapo kwenye viwanja hivyo. Uteuzi wa Gavana Ndulu, Manaibu Gavana, Dkt. Enos Bukuku na Bw.Lila Mkila ulifanyika wakati mipango ya awali ya kujenga nyumba hizi
ilikuwa imeshaanza. Benki Kuu ilikodisha nyumba mbili, mojakiwanja namba 480 Barabara ya Bray, Masaki na nyingine kiwanja namba 591,Msasani Peninsular kwa matumizi ya viongozi hao wawili ambao walikuwa bado wanaishi kwenye nyumba zao mbali na ofisi.
Kati ya Oktoba 2007 aliporipoti kazini kama Naibu Gavana hadi Aprili 2008, Profesa Ndulu aliishi kwenye nyumba yake iliyoko Mbezi Beach, na Naibu Gavana Mkila naye pia aliishi nyumbani kwake kabla ya kuhamia kwenye nyumba hizi zilizokodishwa.
Benki Kuu iliamua kumhamisha Naibu Gavana Juma Reli kwenda Barabara ya Mahando Masaki ili kuruhusu matengenezo ya nyumba aliyokuwa anaishi Kinondoni Barabara ya Msese. Naibu Gavana Dkt.Bukuku anaishi kwenye nyumba yake na Benki Kuu inatoa posho ya nyumba kulingana na mkataba.
Nyumba hizo mbili zilizojengwa chini ya miradi iliyotajwa, sasa hivi zimekamilika.Gavana wa Benki Kuu, Profesa Ndulu alihamia nyumba namba 12 Barabara ya Tumbawe Desemba 17,2009 na Naibu Gavana Mkila alihamia nyumba namba 57 Mtwara Crescent Desemba 4,2009
Kama ilivyo kiutaratibu, ukaguzi wa mahesabu yanayohusu miradi hiyo utafanyika kisheria. Kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya mwaka 2006, Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) ndiye mkaguzi wa mahesabu ya Benki Kuu; ambaye ameanza kufanya kazi hii tangu mwaka 2007. Yeye ameiteua kampuni ya Ernst & Young kama wakaguzi wa kumsaidia kutekeleza jukumu hili.
IMETOLEWA NA IDARA YA UHUSIANO NA UMMA NA ITIFAKI
BENKI KUU YA TANZANIA
SEPTEMBA 30, 2009
Bank of Tanzania Executive officers are entitled to official residence provided by the Bank. Initially the Bank used to have only two executive officers, the Governor and one Deputy Governor. The Governor was living at BOT house No. 387 Mahando Street and Deputy Governor at BOT house No. 43 Msese Road. As a result of the changes made in section 8 of the Bank of Tanzania Act, 2006, the Bank has now four Executives, the Governor and three Deputy Governors, for whom it is obliged to provide official accommodation.
In 2006, in advance of the presidential appointment of the current office bearers, the Bank decided to construct two additional executive accommodations, one on plot No. 12 Tumbawe Road and another on plot No. 57 Mtwara Crescent at Oysterbay, Dar es Salaam. A team of consultants led by M/S SKY Architects Consultants was engaged to provide schematic drawings that were reviewed by the Bank and two of these, one for each plot, were selected for detailed design stage.
Each residence was designed to be a one storey building with five bedrooms, visitors lounge, family lounge, dining area and associated service rooms. The outbuildings include servant’s quarter, car ports, swimming pool, boundary wall, security systems and guard house. Services include power generator, central cooling system and water storage facilities while external works include landscaping and paved car park.
The consultants then prepared bills of quantities and technical specification that were compiled to form tender documents ready for tender process. All procedures in line with procurement laws and regulation were adhered to, when determining the cost of each of the residences as well as in selecting contractors and sub contractors. Each residence was considered as an independent project and a separate tender process was carried out for each one.
It is important for the public to know that, the planning and decision to have these houses constructed was done before Prof Benno Ndulu was appointed at the Bank of Tanzania.
Tenderers for works at plot No. 12 Tumbawe Street were invited using competitive open tender advertised on the Daily News of 26th February 2008. Interested contractors of class II and above were invited to apply for tender document and were instructed to pay non-refundable tender fee of Tshs 50,000/=.
A total of 12 contractors applied and collected the tender documents, but only 10 submitted their bids before deadline, 25th March 2008. The received tenders were opened by BOT Tender Board and forwarded to Project Consultant via the Bank of Tanzania Estate Management Department for evaluation. Tender results read during tender opening ranged from the lowest tender price of Tshs 1,399,184,549.00 to the highest price of Tshs 1,847,763,537.00.
After tender evaluation, which involved preliminary examination of tender, arithmetic correction and detailed analysis, the lowest evaluated bidder was determined to be M/s Electrics International Co. Limited at a corrected tender price of Tshs 1,274,295,025.26. Evaluation report was deliberated by BOT Tender Board and it was approved to award construction works to M/s Electrics International Co. Limited at a fixed contract price of Tshs 1,274,295,025.26 and 32 weeks completion period.
Contract agreement between the Bank and the contractor was signed on 3rd June 2008 and construction works started immediately thereafter. Subcontractors for specialized works were nominated and approved by the BOT Tender Board. These included M/s Remco (International) Ltd for Air Conditioning installation, M/s Ginde EAP Services Ltd for plumbing and drainage systems and M/s Pomy Engineering Co. Ltd for Electrical installations. All these companies are registered in Tanzania.
Tenderers for house no. 57 Mtwara Crescent were invited through a competitive tender method where 5 short-listed contractors were invited to collect tender documents and bid for work. Submitted tenders went through the same tender process detailed above that resulted into M/s Holtan Builders Ltd being determined the lowest evaluated bidder at Tshs 1,272,348,512.00 and 24 weeks completion period.
Subcontractor nominated and approved in this case were M/s Jandu Construction & Plumbers Ltd for plumbing and drainage systems, M/s Barkley Electrical Contractors Ltd for electrical installation and M/s Remco (International) Ltd for Air Conditioning installation. The cost for specialized works undertaken by subcontractors for each site is included on the fixed contract prices for respective main contractor. Likewise, lists of project parties for both works are displayed on the sign boards that are still erected at the front side of respective plots.
While the two projects were still on preliminarily stages, appointment of the three new executive officers to Bank of Tanzania was completed. The Bank was thus compelled to rent two residential houses one on plot No. 480 Bray Road Masaki and another on plot No. 591 at Msasani Peninsular.
One house was allocated to Professor Benno Ndulu, by then the first Deputy Governor, and another to Deputy Governor Lila Mkila. Prior to moving to this rented house; between October 2007 and April 2008, Prof Ndulu lived in his own house in Mbezi Beach. Likewise Deputy Governor Mkila stayed in his own house before moving to the rented premise.
These movements were to facilitate easy access to the office in light of traffic congestion in the city. It was decided to relocate Deputy Governor Juma Reli to house No. 387 Mahando Street to give way for planned refurbishment required at house No. 43 Msese road. Deputy Governor Enos Bukuku is residing in his own private house, and is paid housing allowance in lieu of occupying official residence as entitled – pending the planned refurbishment of Plot No. 43 Msese road residence.
The construction of the two executive residences has now been completed. Both Governor Ndulu and Deputy Governor Mkila, who were residing in rented houses have relocated to the new Bank of Tanzania official residences. The Governor has relocated to house No. 12 Tumbawe Road since 17th December 2009 and Deputy Governor Mkila to house No. 57 Mtwara Crescent since 4th December 2009.
As it is with all other Bank of Tanzania projects, these too will be subject to the usual audit process. It might be important for the public to know that, as stipulated in the Bank of Tanzania Act 2006 the Controller and Auditor General (CAG) is the external auditor for the Bank. The CAG has retained the services of the Ernst and Young, an international audit firm to support the external audit work of the Bank.
Issued by Public Relations & Protocol Department
BANK OF TANZANIA
30TH DECEMBER 2009
NAOMBA UNISAIDIE KWA KURUSHA HII KWENYE BLOG YAKO, NAMTAFUTA KAKA YANGU AITWAYE RAYMOND FRED MTOI TULIACHANA NAYE MWAKA 2000 ALIPOONDOKA KWENDA UK KWA MASOMO.
NI MIMI NAPENDAEL E.J.
MDAU EA DAR

