Katibu Mkuu katika Wizara ya Uchukuzi Mhandisi Omar Chambo (kulia) akipokea ufunguo wa gari moja lenye thamani ya shilingi milioni 82 za kitanzania kutoka kwa Mkuu wa sekta ya Miundombinu katika jumuiya ya Ulaya ( EU Head of Infrastructure) Mr. Adam Grodzicki (mwenye miwani) kwaajili ya kusaidia sekta ya usafiri katika Wizara ya Uchukuzi

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Mhandisi Omar Chambo akijaribu kuwasha gari moja aina ya TOYOTA Land Cruiser Station Wagon lenye thamani ya shilingi milioni 82 za kitanzania kutoka kwa Msimamizi mkuu wa Sekta ya Miundombinu katika Jumuiya ya Ulaya (EU Head of Infrastructure)Mr. Adam Grodzicki (kulia )kwa ajili ya kusaidia sekta ya usafiri katika Wizara ya Ujenzi iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Gari lililokabidhiwa kwa Wizara ya Uchukuzi leo.
Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 24, 2011

    Mhandisi Omar habari za kazi?.Hizi gharama za hili 'kruza mkonga' kwanini(badala yake) serikali isingeomba hata lori mbili za kuzolea taka jijini Daresalaam.Hili suala la usafi jijini Dar linaweza lisikuhusu moja kwa moja lakini ninachotaka kusema hapa ni kwamba jijini la Daresalaam ni chafu sana.Nyie mnaokaa huko kwenye majiji masafi wenzetu wanafanyaje huko(kila mtu aje na wazo lake)..
    maana Dar ukiweka mapipa ya takataka kila kona ya jiji yanaibiwa!!

    David V

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 25, 2011

    Tatizo kubwa la waTZ ni utamaduni. Utamaduni wetu hautufundishi kufanya kitu kwa hiyari. Kila kitu lazima tusukumwe ndio tufanye. Chukulia wewe mwenyewe nyumbani kwako. Shughuli za usafi zote zinafanywa na mama watoto au dada wa kazi. Ukienda ofisini usafi wa maeneo unafanywa na mfanyakazi wa sehemu ya usafi. Kama usafi haukufanywa na watu waliopangiwa hiyo kazi basi haufanywi na mtu mwengine. Miji yetu tumewapangia manispaa zifanye usafi wa mji, wakiwa hawa wafanyakazi hawakufanya hiyo kazi basi mji unakuwa mchafu. Nchi za wenzetu usafi wa mjini ni jukumu la kila mkaazi wa huo mji. Wakorofi hawakosekani, lakini kuna watu wakikuta takataka zimetupwa hovyo basi waziokota na kuziweka zinapotakiwa kwenye pipa la taka. Kuna miji ukitupa taka sio sehemu yake ni kosa unalipa faini. Kwa hivyo ni kuwa wenzetu wana utamaduni wa kufanya usafi kwa hiyari na kuweka sheria kali kwa wakorofi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...