Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii. 

 Ikiwa ni mwaka mmoja na nusu sasa tangu kufikishwa mahakamani kwa aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, (TRA) Harry Kitilya na wenzake wawili upande wa mashtaka umeieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa shauli hilo bado haujakamilika.

Kitilya pamoja na aliyekuwa miss Tanzania mwaka 1996, ambaye pia alikuwa Ofisa wa benki ya Stanbic, Shose Sinare na Sioi Graham Solomon ambao walifikishwa mahakamani hapo kwa Mara ya kwanza April 1, mwaka jana wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji wa USD Mil.6 

Mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa kesi hiyo leo Novemba 3 ilifikishwa kwa ajili ya kutajwa ambapo Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi ameileza mahakama kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Alidai kuwa bado wanasubiri awamu ya pili ya upelelezi kutoka nchini Uingereza na kuomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi November 10, mwaka huu.

Katika kesi hiyo, washtakiwa wote wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya March 2013 na September 2015 wakati wa mchakato wa mkopo wa dola za Marekani 550 milioni  kwa  serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard Uingereza.

Pia wanadaiwa kuwa  March 2013 jijini Dar es Salaam walijipatia Dola za Marekani 6 milioni, wakionyesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji upatikanaji wa mkopo  na zililipwa kupitia  Kampuni ya Egma T Ltd.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...