Na  Bashir  Yakub.

Badala ya kuendesha shule za kulea watoto kinyemela huko mitaani, makala haya yatakueleza namna ambavyo unaweza kufanya kusajili  na hivyo ukaendesha shughuli hii kihalali.

Ifahamike kuwa ni  kosa la jinai kuendesha kituo au  shule ya kulea watoto  bila usajili. Kanuni ya 4( 1 ) ya Kanuni za Vituo vya Kulea Watoto Wadogo Mchana na Watoto Wachanga za mwaka 2012,  zinasema kuwa mtu hataendesha kituo cha kulea watoto wadogo isipokuwa kama anamiliki cheti halali cha usajili. Kwahiyo epuka kuingia katika kosa hili kwa kusajili kituo chako.Makala yatakuwa yakitafsiri Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009, pamoja na Kanuni za Vituo vya Kulea Watoto Wadogo Mchana na Watoto Wachanga za mwaka 2012.

SIFA ZINAZOHITAJIKA KABLA YA KUOMBA USAJILI.

1.Eneo ambapo  kituo kitajengwa litatakiwa kukaguliwa na afisa afya wa eneo husika na kutoa ripoti ya kuridhisha kuwa panafaa kwa ajili ya kulelea watoto. Hii ni kwa mujibu wa kanuni ya  4(3).

2.  Kama eneo/jengo ambapo utaendeshea kituo ni la kupanga basi hakikisha una mkataba wa pango ambao hauko chini ya miaka mitatu.  Kanuni ya 4(4).
3. Utatakiwa kuthibitisha uwezo wa kifedha kuwa unaweza kuendesha kituo.
4. Hakikisha eneo lina vifaa vya kutosha kwa ajili ya michezo ya watoto. Hii ni kutoka kifungu cha 47(1)( c ).

5. Muombaji/waombaji wawe na akili timamu.

6. Uthibitisho kuwa baada ya kupewa cheti cha kuendesha kituo hautatoa, kuuza, kukodisha  kituo au cheti chako kwa mtu mwingine yeyote.
                   
KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Jana tulikuwa na harambee ya uchangishaji wa ujenzi wa kanisa nitakutumia clip hapa
    .

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...