Maonesho hayo yameanza tarehe 28/06/2019 na yatamalizika tarehe 13/06/2019. Wanachama wa mifuko yote miwili wanaalikwa kuja kupata huduma mbalimbali katika banda namba 13.

NSSF na PSSSF wanashiriki kwa pamoja katika maonesho hayo ili kuweza kutoa huduma ya Hifadhi ya jamii ambapo NSSF inawahudumia wananchi kutoka sekta binafsi na sekta isiyokuwa rasmi na kwa upande wa PSSSF wanawahudumia wanawahudumia watumishi wa umma.

Wanachama pamoja na wadau wa Mifuko hiyo wanatakiwa kutumia fursa hiyo kutembelea banda katika viwanja vya sabasaba

Mabadiliko ya mwaka 2018 katika sekta ya Hifadhi ya jamii yalifuta ushindani katika sekta hiyo. Hivyo wananchi wanaandikishwa kwenye mifuko hiyo kulingana na sekta waliopo.
Meneja Kiongozi wa Uhusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF Bi Lulu Mengele akitoa elimu kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na NSSF katika banda la NSSF na PSSSF katika maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa. 
Afisa Uhusiano wa NSSF Bi Aisha Sango akitoa ufafanuzi kwa mgeni alietembelea banda la NSSF na PSSSF katika maonesho yanayoendelea ya kimataifa ya Sabasaba katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa. 
Meneja Kiongozi wa Uhusiano na Elimu kwa Umma wa PSSSF Bi Eunice Chiume akitoa elimu kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na PSSSF  katika banda la NSSF na PSSSF wakati wa  maonesho yanayoendelea  ya kimataifa ya  Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa. 
Afisa matekelezo wa NSSF Ndugu Abdulaziz Abeid akitoa ufafanuzi kwa mgeni alietembelea banda la NSSF na PSSSF katika maonesho yanayoendelea ya kimataifa ya Sabasaba katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa.
Maafisa Uhusiano wa NSSF (Aisha Sango, Kushoto na Amani Marcel, Katikati) na wa PSSSF (Coleta Mnyamani) wakitoa elimu kwa wageni mbalimbali kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na Mifuko hiyo katika maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa. 
Afisa Uhusiano wa PSSSF ndugu Abdul Njaidi akitoa ufafanuzi kwa mgeni alietembelea banda la NSSF na PSSSF katika maonesho yanayoendelea ya kimataifa ya Sabasaba katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...