Mtaalam Mwezeshaji kutoka Benki ya Dunia, Bw. Waleed Malik akitoa maelezo kuhusu Mahakama Inayotembea inavyofanya kazi, wakati wa mafunzo kwa vitendo kwa watumishi wanaofanya kazi kwenye Mahakama hiyo, yaliyofanyika leo kwenye Kituo cha Mafunzo na Habari kilichopo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam. (Wa pili kulia) ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania,Mhe Katarina Revocati(wa tatu kwanza kushoto) ni Msaidizi wa Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Upendo Ngitiri, (wa pili kushoto) ni Mkurugenzi wa Menejimenti ya Mashauri wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya, (wa tatu kushoto) ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya DaresSalaam. (Wa nne kushotoni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Bw. Leonard Magacha na watano ni Naibu Msajili Mwandamizi Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Messeka Chaba.


Msajili Mkuu wa Mahakama Tanzania, Mhe. Katarina Revocat akifungua mafunzo kwa vitendo kuhusu Mahakama Inayotembea kwa baadhi ya watumishi wa Mahakama ya Tanzania, yaliyofanyika leo katika Kituo cha Mafunzo na Habari kilichopo, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Bw. Kalege Enock (aliyenyoosha kidole) akiwaonyesha baadhi ya viongozi wa Mahakama ya Tanzania na watumishi wanaofanya kazi katika Mahakama Inyotembea moja ya kifaa kilichopo ndani ya gari la Mahakama hiyo, wakati wa mafunzo kwa vitendo yaliyofanyika leo katika Kituo cha Mafunzo na Habari kilichopo katika Mahakama Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.
Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revokati (katikati)akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Mahakama ya Tanzania wanaofanya kazi katika Mahakama Inayotembea(Makao Makuu) mara baada ya kufungua mafunzo kwa vitendo kwa watumishi hao. (Kushoto wa kwanza) ni Mkuu wa Kitengo cha Maboresho ya Mahakama ya Tanzania (JDU), Mhe. Zahra Maruma, (wa pili kushoto) ni Mkurugenzi wa Menejimenti ya Mashauri wa Mahakama ya Tanzania,Mhe. Eva Nkya na (Watatu kushoto) ni Mtaalam Mwezeshaji kutoka Benki ya Dunia, Bw. Waleed Malik. Kulia wa kwanza ni Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mhe. Kelvin Mhina, wa pili kushoto ni Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Messeka Chaba na (wa tatu kulia) ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Bw. Leonard Magacha.

(Picha na Mary gwera na Magreth Kinabo )

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...